STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 22, 2013

Mbwana Samatta azidi kung'ara Afrika

Mbwana Samatta alipokuwa akiitumikia Stars dhidi ya Morocco

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ameendelea kung’ara katika michuano ya Afrika, baada ya mwishoni mwa wiki kuifungia timu yake ya TP Mazembe ya DR Congo bao lililoipa sare ya 1-1 ugenini dhidi ya ESS ya Algeria.
Katika pambano hilo lililochezwa Ijumaa kwenye uwanja wa Mei 8, 1945 la ufunguzi wa hatua ya Makundi Kombe la Shirikisho Afrika kwa kundi B, wenyeji walilazimika kulichomoa bao hilo la Samatta.
Samatta alifunga bao hilo katika dakika ya 81 , lakini hata hivyo dakika mbili baadaye wenyeji walichomoa kupitia kwa beki wao Mourad Delhoum.
TP ya Samatta sasa itarejea nyumbani kuisubiri FUS Rabat ya Morocco katika pambano lao litakalochezwa mjini Lubumbashi Agosti 4.

No comments:

Post a Comment