STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 22, 2013

Afande Sele kuweka Dini videoni


Afande Sele akiwajibika jukwaani
MKONGWE wa muziki wa hip hop nchini, Seleman Msindi 'Afande Sele' yupo katika harakati za kufyatua video ya wimbo wake mpya unaoendelea kutamba kwenye vituo vya redio uitwao 'Dini Tumeletewa'.
Afande Sele aliiambia MICHARAZO kuwa ijapokuwa hivi sasa yupo mapumzikoni kuupisha mfungo wa mwezi wa Ramadhani, lakini bado anaendelea na mipango ya kukamilisha video ya wimbo huo ili kukata kiu ya mashabiki wake ambao wengi wamekuwa wakiiulizia mara kwa mara.
"Niko mbioni kutoa video ya wimbo Dini Tumeletewa nilioimba na Belle 9. Ikikamilika itasambazwa ili mashabiki wa muziki washuhudie kile nilichoimba,"alisema Afande.
Katika hatua nyingine, Afande Sele alisema kuwa tangu atoe wimbo huo amekuwa akipokea pongezi nyingi na kuombwa atoe video yake.
Msanii huyo amekuwa akijizolea sifa kemkem kutokana na nyimbo zake nyingi kuwa na mashairi yenye kugusa hali halisi ya maisha ya Mtanzania.

No comments:

Post a Comment