STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 9, 2016

Ronaldo kamili gado kuanza mambo La Liga

http://www.ronaldo7.net/news/2014/04/824-cristiano-ronaldo-fitness-drills.jpgUSIYEMPENDA Kaja. Ndivyo ambavyo Osasuna watakuwa wanawaza sana, baada ya kuwepo kwa taarifa kwamba nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo yupo fiti na kesho huenda akashuka uwanjani kuvaana nao.
Straika huyo amebainisha kuwa atarejea uwanjani Jumamosi hii katika mchezo dhidi ya Osasuna.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 31 amekuwa akijiuguza goti lake katika majeruhi aliyopata katika mchezo wa fainali ya michuano ya Ulaya hali iliyomfanya kukosa mechi ys Super Cup ya Ulaya na zingine walizocheza Madrid katika La Liga msimu huu. Akihojiwa kuhusiana na hali yake inavyoendelea, nahodha huyo wa Ureno amesema yuko tayari kurejea uwanjani na anatarajia kucheza katika mchezo dhidi ya Osasuna.
Madrid wameshinda mechi zao zote mbili za la Liga walizocheza msimu huu, kwa kuzifunga Real Sociedad na Celta Vigo.

No comments:

Post a Comment