STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 9, 2016

Wilshere mbona mtamu, subirini tu muone-Wenger

http://www.telegraph.co.uk/content/dam/football/2016/04/07/jack-wilshere8-large_trans++qVzuuqpFlyLIwiB6NTmJwfSVWeZ_vEN7c6bHu2jJnT8.jpgMBONA freshi tu! Kocha wa klabu ya NEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amedai kuwa Jack Wilshere anaweza kuitumikia klabu hiyo kwa kipindi kirefu mbele ya safari huku akisisitiza kuwa kiungo huyo hana chochote cha kumuonyesha zaidi ya kuwa fiti. Wilshere ameenda kwa mkopo wa msimu mzima katika klabu ya AFC Bournemouth dakika za mwisho kabla ya dirisha la usajili majira ya kiangazi halijafungwa ikiwa kama sehemu ya mikakati ya kujijenga upya kufuatia kusumbuliwa na majeruhi ya mara kwa mara katika misimu miwili iliyopita.
Akizungumza kuelekea mchezo wao wa Ligi Kuu dhidi ya Southampton, Wenger alipuuza habari kuwa amekuwa haelewani na kiungo huyo mwenye umri wa miaka 24 ambaye amekuwa akimtaja kuwa na uwezo mkubwa.
Kocha Wenger alisema alizungumza na Wilshere naye alimwambia hadhani kama ataweza kupata muda wa kutosha kucheza akibakia hapo kwa vile anataka  kucheza zaidi msimu huu baada ya kupona majeruhi yake.
Wengeraliendelea kudai kuwa alimruhusu kuondoka kwasababu alikuwa hawezi kumuahidi muda wa kutosha wa kucheza kama alivyotaka mwenyewe.

No comments:

Post a Comment