STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 9, 2016

Nyie vipi, Ngoma? Mambo yapo kwa Bocco baba'ake

http://www.cecafafootball.org/wp-content/uploads/2014/03/john-bocco.jpg
John Bocco akishangilia moja ya mabao yake
Na Tariq Badru

KUELEKEA raundi ya nne ya Ligi Kuu Bara, nahodha wa Azam, John Bocco 'Adebayor' amewafunika mapro wa kimataifa wa klabu za Simba na Yanga katika mbio za kuwania kiatu cha dhahabu.
Bocco ambaye yupo jijini Mbeya akiwa na kibarua cha kuiongoza tena timu yake kusaka pointi tatu ugenini dhidi ya Wagonga Nyundo wa jiji hilo, mpaka sasa ana mabao matatu akiongoza orodha ya wafungaji.
Straika huyo ngongoti amewaacha mbali kina Amissi Tambwe, Donald Ngoma wa Yanga ambao msimu uliopita walitisha kwa kutupia kambani ambao mpaka sasa hawana bao hata lile la kuotea katika msimu huu wa ligi hiyo.
Mbali na nyota hao wa Yanga, Bocco pia amemzima Laudit Mavugo aliyetabiriwa mapema kusumbua nchini kutokana na rekodi yake ya mabao nchini Burundi ambapo baada ya mechi tatu za ligi hiyo ametupia mabao mawili akiwa na Simba.
Straika mwingine wa kimataifa wa Simba aliyeachwa solemba na Bocco ni Frederick Blagnon mwenye bao moja, huku mapro wengine wa wazawa waliopo klabu tofauti 16 za ligi hiyo wakiwa hawana chao mbele ya Bocco.
Bocco ambaye hana hulka ya kujisifu wala kuzungumza sana kwenye vyombo vya habari amekuwa akisema mwanzo alioanza nao ni kudra za Mungu anayemshukuru na ameapa kupambana akishirikiana na wenzake kurejesha taji la Ligi Kuu Azam.
Azam ndiyo inayoonga msimamo wa ligi kwa sasa ikilingana kila kitu na Mbeya City watakaovaana nao kesho kwenye Uwanja wa Sokoine, zote zikiwa na pointi saba na mabao matano ya kufunga na kufungwa moja, wakifuatiwa na Simba yenye pointi kama hizo na mabao matano ya kufungwa ila imefungwa mabao mawili.
 

Orodha kamili ya wafungaji ipo hivi kwa sasa;
3- John Bocco                            (Azam)
2- Rashid Mandawa        (Mtibwa Sugar)
    Rafael Daud                   (Mbeya City)
    Laudit Mavugo                      (Simba)
1- Federick Blagnon                  (Simba)
    Shiza Kichuya                       (Simba)
    Subianka Lambert                (Prisons)
    Omar Mponda                     (Ndanda)
    Shaaban Kisiga         (Ruvu Shooting)
    Hood Mayanja              (African Lyon)
    Wazir Junior                 (Toto African)
    Mudathir Yahya                      (Azam)
    Abdallah Seseme                ( Mwadui)
    Victor Hangaya                    (Prisons)
    Frank Msese              (Ruvu Shooting)
    Shomari Ally               (Mtibwa Sugar)
    Shija Mkina                         (Ndanda)
    Deus Kaseke                          (Yanga)
    Simon Msuva                         (Yanga)
    Juma Mahadhi                       (Yanga)
    Haruna Shamte              (Mbeya City)               
    Salim Mbonde             (Mtibwa Sugar)
    Bahati Ngonyani                 (Majimaji)
    Ramadhani Chombo        (Mbeya City)
    Omar Ramadhan             (Mbeya City)
    Emmanuel Kichiba                  (Mbao )
    Ally Ramadhani           (Kagera Sugar)
    Adam Kingwande              (Stand Utd)
    Ibrahim Ajib                          (Simba)
    Abdulrahman Mussa   (Ruvu Shooting)
    Kipre Balou                             (Azam)

No comments:

Post a Comment