STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 9, 2016

Buriani Kocha Mohammed Hassan Msomali

Kocha Mohammed Hassan 'Msomali' enzi za uhai wake hivi karibuni
Msomali wa kwanza kushoto waliochuchumaa enzi za uhai wake akikipiga Cosmopolitan
ALIYEKUWA Kocha mkongwe na mwenye mafanikio makubwa nchini, Mohammed Hassan 'Msomali' (74) amezikwa leo mjini Morogoro baada ya kufariki dunia jana mchana nyumbani kwake mjini humo.
Marehemu aliyewahi kuzichezea Yanga, Cosmo na Taifa Stars kwa mafanikio makubwa kabla ya kuzinoa timu za Tumbaku, Mseto, Pan Africans na Moro United sambamba na timu za Mkoa wa Morogoro na Taifa Stars, atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika soka la Tanzania.
Ukiondoa kuwa miongoni mwa walioisaidia Cosmo kubeba taji la Ligi ya Tanzania mwaka 1968 wakiipoka Simba (enzi za Sunderland) iliyokuwa ikimiliki taji kwa miaka miwili tangu kuanzishwa kwa Ligi hiyo mwaka 1965, pia ndiye kocha wa kwana kubeba taji kwa timu za mkoani.
Alifanya hivyo mwaka 1975 akiwa na Mseto ya Morogoro na kubeba tena akiiongoza Pan Africans mwaka 1982.
Kocha huyo ndiye aliyewaibua nyota mbalimbali waliowahi kutamba na kuendelea kuwa kiigizo chema kwa wanasoka wa kisasa kama Zamoyoni Mogella, Malota Soma, John Simkoko, Omar Hussein, na kikosi cha dhahabu cha Pan Africans wakiongozwa na kipa Juma Pondamali, Sunday Manara, Mohammed Mkweche, Mohammed Yahya 'Tostao' Mohammed Rishard Adolph, Jafar Abdulrahman, Ally Katolila na wengine.
Mwaka jana kocha huyo aliyekuwa kiungo mahiri na aliyeiwakilisha Tanzania kwenye michezo ya Afrika (All Africa Games) mwaka 1973 ilipofanyikia Nigeria, alienda kuhiji Makka kwa maana hiyo mautio yamekumta akiwa ni ALHAJI.
Innalillah Waina Illaiy Rajiun. Tangulia mzee wetu Mohammed Msomali, nasi tu nyuma yako. Blog hii ya Micharazo Mitupu inatoa pole kwa ndugu, jamaa, familia na rafiki wa marehemu Msomali sambamba na wadau wa soka kwa kuwakumbusha kuwa kila nafsi itaonja mauti.Tumuombee katika safari yake ya Ahera nasi tukijiandaa kwa safari hiyo kwa vile hatujui saa, siku wala mwaka.

No comments:

Post a Comment