STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 18, 2013

Yanga, Mgambo JKT wavuna Mil 24 Mkwakwani

Hamis Kiiza alipokuwa akiwania mpira na beki wa Mgambo JKT juzi kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga


Na Boniface Wambura
PAMBANO la  Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Mgambo Shooting na Yanga lililochezwa jana (Aprili 17 mwaka huu) Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga limeingiza kiasi cha sh. 24,865,000 kutokana na watazamaji 4,386.

Viingilio katika mechi hiyo namba 162 iliyomalizika kwa timu hizo kutoka sare ya bao 1-1 vilikuwa sh. 10,000 kwa jukwaa kuu na sh. 5,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 5,547,337.50 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 3,792,966.10.

Asilimia 15 ya uwanja sh. 2,820,680.08, msimamizi wa kituo sh. 120,000, kamishna wa mechi sh. 90,000, waamuzi sh. 270,000, maandalizi ya uwanja sh. 100,000 na tiketi sh. 1,587,500.

Mgawo mwingine ni gharama za mechi sh. 1,692,408.05, Kamati ya Ligi sh. 1,692,408.05, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 846,204.05 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Tanga (TRFA) sh. 658,158.69.

No comments:

Post a Comment