STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 6, 2014

Dokii, Anita wa Mwanza waja na mpya


MUIGIZAJI nyota wa filamu nchini, Ummy Wenceslaus 'Dokii' anajiandaa kuingiza sokoni filamu mpya iitwayo 'I Love Mwanza' aliyoizalisha akishirikiana na 'shoga' yake ambaye ni Rais wa Wasanii jijini Mwanza afahamikaye zaidi kama Anita.
Akizungumza na MICHARAZO Dokii alisema filamu hiyo imekamilika kitambo kirefu na kwa sasa ipo kwenye mchakato wa kuachiwa mtaani ikiwashirikisha wasanii mchanganyiko wakiwamo wakongwe na chipukizi wa mikoa ya Dar na Mwanza.
Dokii aliwataja baadhi ya wasanii walioshiriki filamu hiyo inayokuwa kazi yake mpya baada ya kuuza sura kwenye filamu ya 'Mdundiko' ni pamoja na yeye Dokii, Anita ambaye ni prodyuza anayekuja juu nchini kwa sasa kutokea Mwanza, Kulwa Kikubwa 'Dude', Sabrina Rupia 'Cathy', Kiwi, Fred na chipukizi wa jijini Mwanza.
"Ni moja ya filamu ya kusisimua yenye makali kama 'Mdundiko' iliyotwaa tuzo ya kimataifa nchini Marekani, kazi hii nimezalisha mimi na rafiki yangu Anita na imeshirikisha wasanii kadhaa nyota na chipukizi nchini," alisema.
Dokii, alisema anawaomba mashabiki wa filamu nchini kukaa mkao wa kula kupata burudani kupitia kazi hiyo ambayo ina ujumbe na mafunzo makubwa kwa jamii.

No comments:

Post a Comment