STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 6, 2014

Uholanzi yapata pigo, Van Persie naye aumia

MSHAMBULIAJI wa Uholanzi, Robin Van Persie sasa atatakiwa kumuona daktari baada ya kuumia nyonga akiichezea timu yake hiyo juzi  katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Wales mjini Amsterdam.
Wazi kocha Louis Van Gaal atakuwa anaumia sana kichwa kwa maumivu ya mshambuliaji huyo wa Manchester United, zikiwa zimebaki siku zisizozidi 10 kabla ya kucheza na Hispania katika mchezo wa ufunguzi wa Kombe la Dunia.
Kabla ya kuumia na kutoka, Van Persie alitengeneza bao la kwanza lililofungwa na Arjen Robben wakati bao la pili lilifungwa na Jeremain Lens.

No comments:

Post a Comment