STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 6, 2014

TOT Band waingia studio kufyatua mpya

Redock Mauzo
BENDI ya TOT 'Vijana Fashion' wanatarajia kuingia studio wiki ijayo kurekodi nyimbo zao mbili wakianza na 'Akili ni Mali' kabla ya kumalizia 'Maisha Duni'.
Akizungumza na MICHARAZO kiongozi wa bendi hiyo Redock Bokassa 'Redock Mauzo' alisema wataingia studio za Amaroso, zilizopo jijini Dar es Salaam.
Redock alisema wataanza kazi hiyo wiki ijayo kwa kibao cha 'Akili ni Mali' alioutunga yeye na baada ya hapo watamalizia wimbo wao wa pili wa 'Maisha Duni' wa Frank Kabatano kabla ya kuendelea na nyimbo nyingine zinazoendelea kutungwa sasa kwa ajili ya kukamilisha albamu yao mpya.
"Vijana wa Fashion, tunatarajia kuingia studio za Prodyuza Amoroso kuanza kurekodi nyimbo zetu mpya, kazi hiyo itaanza wiki ijayo kwa wimbo wa 'Akili ni Mali'," alisema.
Rapa na muimbaji huyo aliyekuwa Extra Bongo kabla ya kurejea TOT Band, alisema wamepania kurejesha heshima ya bendi hiyo iliyowahi kutikisa anga la muziki wa dansi kwa vibao murua vilivyokuwa kwenye albamu zao kadhaa ikianzia 'Mtaji wa Maskini'.

No comments:

Post a Comment