STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 6, 2014

Tanzania yapaa viwango vya FIFA, Algeria yaiengua Ivory Coast

Kikosi cha Taifa Stars kilichoiwzesha Tanzania kupaa kwenye viwango vya FIFA kwa kuzitoa nishai Zimbabwe na Malawi
TANZANIA imepaa katika viwango vya Soka vya Fifa kwa nafasi tisa huku ikiishusha Zimbabwe kwa nafasi moja baada ya kuitoa katika michuano ya kuwania kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika nchini Morocco 2015.
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), iliifunga Zimbambwe bao 1-0 Uwanja wa Taifa kabla ya kurudiana nchini Zimbabwe na kulazimisha sare ya 2-2, hivyo kuitoa kwa jumla ya mabao 3-2.
Katika viwango vilivyotangazwa jana na Fifa, Tanzania ambayo ilikuwa ikishika nafasi ya 122, imepanda hadi nafasi ya 113 wakati Zimbabwe ikishuka kutoka nafasi ya 98 hadi 99.
Msumbiji ambayo itakutana na Tanzania Julai 20, mwaka huu katika mechi ya kuwania kufuzu Afcon, imeporomoka kwa nafasi nne kutoka 114 hadi 118.
 Kwa upande wa Afrika Mashariki, Uganda ndiyo inayoongoza ikibaki nafasi ya 86 iliyokuwa mwezi uliopita huku Kenya licha ya kushuka kwa nafasi mbili kutoka 106 hadi 108 ikishika nafasi ya pili.
Rwanda imepaa kwa nafasi 15 na sasa inashika nafasi ya 116 huku Burundi ikiporomoka kwa nafasi tatu hivyo kushika nafasi ya 128.
Miamba itakayoliwakilisha Bara la Afrika kwenye fainali za Kombe la Dunia, Algeria ndiyo kinara ikipanda kwa nafasi tatu hivyo kushika nafasi ya 22 duniani ikifuatiwa na Ivory Coast ambayo ni ya 23 baada ya kushuka kwa nafasi mbili.
Ghana imepanda nafasi moja na sasa ni ya 37, Nigeria imebaki nafasi yake ya 44 ya mwezi uliopita huku Cameroon ikiwa ni 56 baada ya kushuka kwa nafasi sita.
Kumi bora ya viwango hivyo, Hispania ndiyo inayoongoza ikifuatiwa na Ujerumani, Brazil, Ureno, Argentina, Uswis, Uruguay, Colombia, Italia na England ikifunga orodha hiyo.

No comments:

Post a Comment