STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 6, 2014

Chamberlain aitia hofu England kuelekea Fainali za Kombe la Dunia

KIUNGO wa kimataifa wa Uingereza, Alex Oxlade-Chamberlain anatarajiwa kufanyiwa vipimo katika goti lake kufuatia kuzuka hofu kuwa alipata majeraha katika msuli wa ndani ya goti. 
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 20 alitolewa nje kufuatia kukwatuliwa na Carlos Gruezo wakati wa mchezo wa kujipima nguvu kati ya Uingereza na Ecuador ambao ulimalizika kwa sare ya mabao 2-2.
Kocha wa timu ya taifa ya Uingereza, Roy Hodgson amesema itakuwa pigo kubwa kama wakimpoteza kinda huyo kwenye michuano ya Kombe la Dunia iliyo mbele yao kwani ni mmoja kati ya wachezaji anaowategemea katika kikosi chake. 
Uingereza inatarajiwa kucheza mechi yake ya ufunguzi dhidi ya Italia Juni 14 mwaka huu huko Manaus. 
Timu hiyo imeshampoteza winga wake Tim Walcot ambaye aliumia naye goti na hivyo kumkosesha michuano hiyo ya Kombe la Dunia inayoanza Alhamisi ijayo.
T

No comments:

Post a Comment