STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 6, 2014

Aliyembunia Rihanna gauni lililozua gumzo alonga

TANGU Rihanna alipotinga katika zulia jekundu la tuzo za mitindo ya mavazi za CFDA na kupozi kwa picha Jumatatu, mitandao ya internet imetawaliwa na mijadala kuhusu chaguo lake la kivazi alichoibuka nacho siku hiyo ambacho ni cha nyavu nyavu na kilichokuwa kikianika kila kilicho ndani.
Ipo sababu iliyomfanya kimwana huyo akapewa tuzo ya Fashion Icon Award 2014, na Adam Selman ambaye alimbunia gauni hilo ndiye pekee anayeweza kufafanua ni kwanini.
Selman amefanya mahojiano na jarida la ELLE na kueleza kwanini alimtengenezea gauni la aina ile.
Katika mahojiano hayo, Selman alibainisha kwamba gauni lile lilitumia siku saba kukamilika huku watu 20 wakihusika kulitengeneza. Licha ya kwamba gauni hilo limetumia siku saba kukamilika, Selman amesema wazo hilo lilikuja mwezi mzima uliopita.
"Tulikuwa mjini Los Angeles na Rihanna kwenye tuzo ya MTV Movie Awards kama mwezi uliopita na sote tukaanza kujadili kuhusu tuzo za CFDA," alisema. "Tukaafikiana wazo la kutengeneza gauni kama lile. Kisha jambo lililofuata nikachora mchoro wa gauni lenyewe. Rihanna akaliidhinisha na kazi ikaanza!"
Aliongeza kwamba Rihanna alifahamu fika kitu alichohitaji. Mbunifu huyo alisema alitokwa na machozi alipomuona kwa mara ya kwanza Rihanna akiwa ametinga gauni hilo.
Selman akatetea chaguo hilo linaloshambuliwa vikali katika mitandao akisema  "...linawatuliza watu. Alionekana amependeza kwa kila mlima wa mwili aliojaaliwa."

No comments:

Post a Comment