STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 6, 2014

Tanzania yaongoza kwa matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii

TANZANIA imetajwa kama kinara wa matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii na hasa Instagram kutokana na wengi wao kutumia kuweka picha za utupu.
Taarifa hiyo imetolewa na Meneja Uhusiano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Innocent Mungy alipokuwa akihojiwa na Kituo cha Radio One ambapo alisema ni aibu kuona watanzania badala ya kuitumia vyema mitandao ya kijamii wenyewe wamejikita kwenye mambo ya upuuzi.
Mungy alisema Tanzania imetajwa kama kinara wa matumizi mabaya ya mtandao wa Instagram duniani kutokana na kukithiri kutweka picha ziisizo za maadili na kuwaomba watumiaji wa mitandao ya kijamii nchini kuonyesha ustaarabu kwa kuitumia vizuri.
Alisea TCRA wanaendelea kuhimiza watanzania kuepuka kusambaza meseji za chuki na uchochezi pamoja na kutumia mitandao hiyo ya kijamii kudhalilisha watu wengine au kujidhalilisha wenyewe kwani hatua kali zitachjukuliwa dhidi ya wote.
Kauli ya Mungy imekuja siku chache baada ya mmiliki wa mtandao huo kutangaza kufuta picha zote za utupu kutokana na kukerwa na watumiaji wake kutaka kuuharibia mtandao huo.
Mmoja wa waasisi wa mtandao wa kijamii wa Instagram, ameambia BBC kuwa sheria zake kuhusu picha za uchi hazimbagui mtu yeyote.
Kampuni hiyo imekosolewa vikali kwa kwa kuondoa picha za wanawake walio nusu uchi kwenye mtandao huo.
Lakini Afisaa mkuu mtendaji wa mtandao huo wa kijamii, Kevin Systrom, amesema kuwa sheria hizo zinalenga kuhakikisha kuwa vijana na watu wazima wanaotumia mtandao huo wako salama.
Masharti ya matumizi ya mtandao wenyewe, yanasema: 'Mtu haruhusiwi kuweka picha za watu walio nusu uchi na picha zenye mada ya ngono. ''
Matamshi yake yanakuja baada ya mwanawe muigizaji maarufu, Bruce Willis, Scout Willis kuweka picha yake kwenye mtandao huo akiwa nusu uchi bila kitu kifuani.
Picha hiyo iliondolewa kwenye mtandao huo na wamiliki wa mtandao na hapo ndipo malalamiko yalianza kuibuka.
Muimbaji Rihanna, ambaye alikuwa na wafuasi milioni 1.3 aliunga mkono kampeini hiyo kabla ya kufunga akaunti yake.
Wamiliki wa mtandao huo wanasema sheria zinapaswa kufuatwa na kila mtu awe mtu mashuhuri au vinginevyo.
"lengo letu ni kuhakikisha kuwa Instagram, ni mahala salama kwa kila mtu , awe maarufu au la. ''
"tunapaswa kuwa na sheria na kuhakikisha kuwa kila mtu anafuata sheria hizo. Bila shaka tunapata changamoto nyingi lakini tutnaedneklea kusisitiza umuhimu wa sheria kufuatwa, '' alisema Systrom
Huku umaarufu wa mtandao huo ukiendelea kuimarika, mtandao huo umekosolewa kuhusiana na baadhi ya picha zinazochapishwa humo . Pia mtandao wenye umebana baadhi ya maneno yanayohusiana na madawa ya kulevya.
Instagram ilinunuliwa na Facebook mwaka 2012.

No comments:

Post a Comment