STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 6, 2014

Shilole kuendelea kuchuna buzi tu kwa sasa


NYOTA wa filamu na muziki nchini, Zuwena Mohammed 'Shilole' amesema hataharakisha kutoa wimbo mpya kwa sasa kwa vile 'Chuna Buzi' inaendelea kusumbua nchini.
Akizungumza na MICHARAZO, Shilole anayefahamika pia kama 'Shishi', alisema licha ya kuwa tayari ameshaandaa wimbo mpya, hatautoa mapema kwa sababu wimbo wake wa sasa 'Chuna Buzi' upo juu.
Shilole alisema wimbo huo ambao hivi karibuni aliiachia video yake bado unaendelea kutamba na asingependa kuwachanganya mashabiki kwa kutoa kazi mpya kwa sasa.
"Kwa kuwa wimbo wa Chuna Buzi upo juu ukisumbua kwenye vituo vya redio na televisheni, nimeamua 'kuuchuna' kwa kuachia kazi mpya licha ya kwamba tayari nimeshakamilika," alisema.
Shilole alisema wimbo huo mpya atauachia baadaye sana, huku akigoma kutaja jina lake kwa madai ni mapema mno, ila aliwataka mashabiki waendelee kupata burudani ya 'Chuna Buzi' kabla ya kupata ladha nyingine ambaye anaamini itawachengua zaidi.
Mwanadada huyo anayetamba na nyimbo kama 'Paka la Baa', 'Lawama', 'Dude Dada' na 'Nakomaa na Jiji', alisema kila uchao hufikiria namna ya kusuuza nyoyo za mashabiki wake.

No comments:

Post a Comment