STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 6, 2014

Maximo awakabikisha Mkwasa, POndamali Yanga


Kocha Maximo, enzi zkiinoa Stars
KOCHA Marcio Maximo kutoka Brazil, tayari ameupitia mkataba wa kuanza kufanya kazi Yanga na kusema: “Nitaanza kazi na (Charles) Mkwasa pamoja na (Juma) Pondamali.”
Awali kulikuwa na hofu huenda kocha huyo angetaka kutua nchini na msaidizi wake kutoka Brazil lakini sasa atalazimika kuwataja wazawa hao katika benchi lake la ufundi.
Habari za uhakika kutoka ndani ya Yanga zinaeleza Maximo ametumiwa mkataba huo ambao awali ulipitiwa na mwenyekiti wa klabu hiyo, Yusuf Manji na ukatumwa nchini Brazil kupitia mwakilishi wake anayeishi jijini Dar es Salaam na amekubali kushirikiana na Mkwasa na Pondamali.
Suala la kocha msaidizi kutoka Brazil, Yanga na Maximo walikubaliana kuwa, atakapokaa mwaka mmoja na kufanya kazi kwa mafanikio, basi Yanga inaweza kuliangalia hilo kama wamuongeze kwenye benchi la ufundi.
Mwakilishi huyo wa Maximo ambaye amekuwa akisimamia zoezi hilo, ameutuma mkataba huo na Maximo ameupokea na kuupitia.
Habari za uhakika zinaeleza, inachotaka Yanga ni Maximo kupunguza dau lake ambalo alianzia dola 16,000 (zaidi ya shilingi milioni 25) kwa mwezi kabla ya kushuka hadi dola 15,000 (zaidi ya shilingi milioni 24), lakini Yanga imesisitiza inataka ashuke kidogo.
Ahadi nyingine ambazo amepewa Maximo ni nyumba na gari la kutumia pamoja na marupurupu mengine ambayo hayajajulikana.
Championi kama kawaida, ndiyo lilikuwa ni gazeti la kwanza kuandika kuhusiana na ujio wa Maximo, taarifa hiyo ilitoka wiki nne zilizopita.
Iwapo Maximo ataupitia mkataba huo na kuukubali, atatua nchini ndani ya siku nne zijazo na kusaini mkataba huo kabla ya kuanza kazi moja kwa moja.
Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji alisema mbele ya wanachama kwamba yuko katika hatua za mwisho kuhakikisha Maximo anatua nchini.
Maximo atafanya kazi na makocha wazalendo, Charles Boniface Mkwasa na Juma Pondamali na huo ndiyo umekuwa msimamo wa Manji.
Pondamali aliwahi kufanya kazi na Maximo wakati akiwa katika kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars.
Katika majadiliano yanayoendelea kati ya Yanga na Maximo ni pamoja na suala la kipa Juma Kaseja ambaye hakuwa na uhusiano mzuri na kocha huyo wakati akiinoa Stars.
Maximo akimalizana na Yanga na kuanza kazi, rasmi atakuwa amechukua nafasi ya Hans van der Pluijm anayekwenda kupiga kazi nchini Saudi Arabia ambaye pia alichukua nafasi ya Mholanzi mwenzake, Ernie Brandts.
CHANZO NI CHAMPIONI IJUMAA

No comments:

Post a Comment