STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 6, 2014

Msiba tena! Nyota wa zamani Simba, Gebo Peter afariki dunia

Gebo Peter (wa kwanza kushoto mstari wa kati) akiwa na wachezaji wenzake wa Simba enzi za uhai wake
Gebo Peter (wa kwanza kulia) akiwa na baadhi ya wadfau wa soka wakati wa mazishi ya kocha James Kisaka
MSHAMBULIAJI wa zamani wa klabu za Simba, Sigara na Taifa Stars, Gabriel Peter 'Gebo Peter' amefariki dunia usiku wa kuamkia leo.
Habari ambazo MICHARAZO ilizipata mapema asubuhi ya hii zilisema kuwa, Gebo alikumbwa na mauti akiwa amelezwa katika Hospitali ya Taifa ya  Muhimbili alipokuwa amehamishiwa kutoka Hospitali ya Mwananyamala alikokuwa amelazwa kutokana na kuzidiwa na maradhi yhaliyokuwa yakimsumbua.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Wilaya ya Ilala (IDFA) Daud Kanuti, Gebo alikuwa amelazwa Mwananyamala kwa tatizo la tumbo na hali ilinadilika kuwa mbaya ndipo alipohamishiwa Muhimbili jana na kuwa chini ya uangalizi akipumulia mashine.
Enzi za uhai wake Gebo alisifika kwa kufumania nyavu kwa kutumia miguu yake yote miwili pamoja na vichwa, huku akiwa ni mmoja ya washambuliaji waliokuwa wakiiliza sana Yanga kila ilipokutana na timu alizokuwa akizichezea kuanzia Sigara mpaka Simba.
Mpaka mauti yanamkumba nyota huyo wa zamani ambaye ni mdogo wa nyota mwingine na shujaa wa Tanzania wa mwaka 1980, Peter Tino alikuwa mmoja wa viiongozi wa timu ya Manyema Rangers na kisoka aliwahi kuzichezea timu za Bora, Safari Contractors, Pan Africans, Sigara, Yanga na Kajumulo World Soccer
Taratibu za mazishi zinaendelea kufanywa na msiba unaelezwa upo nyumbani kwa Vingunguti.
MICHARAZO inatoa pole kwa ndugu, jamaa na familia nzima ya marehemu kwa msiba huo mzito na inawatakia kuwa na Subira katika kipindi hiki kigumu kwa kukumbuka kuwa kila nafsi ni lazima ionje mauti na BWANA Ametwaa na Yeye Ndiye Aliyetwaa Jina lake Lihimidiwe.

No comments:

Post a Comment