STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 6, 2014

Vijana Simba, Yanga kuchuana Rolling Stone

Simba
JUMLA ya timu 27 zinatarajiwa kushiriki katika michuano ya soka ya vijana ya Rolling Stone itakayoanza Julai 4, mwaka huu jijini Dar es Salaam ikishirikisha timu za Ukanda wa Maziwa Makuu.

Mratibu wa mashindano hayo, Willbroad Alphonce, alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa michuano hiyo itafanyika kwa siku 10 na mechi zitakuwa zikichezwa kwenye viwanja vitatu.

"Tunawaandikia barua TFF (Shirikisho la Soka Tanzania) kuomba Uwanja wa Karume, Azam na wamiliki wa Uwanja wa TCC Sigara. Tunaamini watatukubalia kwa ajili ya kuendeshea michuano hiyo," alisema mratibu huyo.

Alisema tayari wameshapata kibali kutoka TFF kuendeshea michuano hiyo jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuibua vipaji vya vijana na timu nyingi zinaweza kupata wachezaji kupitia mashindano hayo.

Alisema michuano hiyo imewaibua wachezaji wengi wakiwamo Amir Maftaha, Salvatory Ntebe na wengine wengi ambao waliitwa kwenye timu za taifa za vijana, hivyo ni wakati wa viongozi wa timu za ligi kuu, daraja la kwanza na timu za Taifa kutumia michuano hiyo kwa ajili ya kupata wachezaji.

Alizitaja timu ambazo zitashiriki kuwa ni Burundi ambao watatoa timu mbili, Kongo (1), Rwanda (1), Uganda (2), Kenya (2), Zanzibar (2) na Tanzania timu zitakazoshiriki ni timu B za Simba, Yanga, Azam FC, Coastal Union, Mtibwa Sugar na Ruvu Shooting.

Nyingine kwa Tanzania ni mabingwa watetezi Eagle Rangers ya Tanga, Mbasco ya Mbeya, Moro, Alliance ya Mwanza na TSC, na kwa mkoa wa Arusha ni Rolling Stone, Vishop Dan, Youth Talent na Bom Bom ya Dar es Salaam.

Alphonce alisema timu zote zipo katika maandalizi shadidi kuhakikisha michuano hiyo inakuwa na upinzani mkali.

Pia aliwaomba wadhamini mbalimbali wajitokeze kudhamini michuano hiyo, kwani bado waandaaji michuano hiyo wanahangaika kutafuta udhamini ili kuyafanikisha.

No comments:

Post a Comment