STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 6, 2014

Nisha huyoo mtaani, Kajala ana laana bhana!

Salma Jabu 'Nisha' katika pozi. Msanii huyo anajiandaa kuiachia filamu yake mpya ya Zena na Betina siku ya Jumatano ijayo
Kajala Masanja anayejiandaa kuitoa Laana kupitia kampuni yake ya Kay Films Production

WAKATI Salma Jabu 'Nisha' akijiandaa kuingiza sokoni filamu yake mpya ya 'Zena na Betina' keshokutwa kisura mwingine wa Bongo Movie, Kajala Masanja, yupo mguu sawa kutoa kazi yake ya kwanza binafsi iitwayo 'Laana'.
Muongozaji mkuu wa filamu hizo, Leah Richard 'Lamata' aliliambia MICHARAZO kuwa, filamu ya Nisha itatoka Juni 12 wakati ile ya Kajala itatoka mwishoni mwa mwezi huu.
Lamata alisema filamu ya Zena na Betina ambayo ni comedian serious ni moja ya filamu tamu kama kazi nyingine alizowahi kuziandikia miswada, kutungia hadithi zake au kuziongoza.
"Filamu ya 'Zena na Betina' na Nisha inatarajiwa kuingia sokoni Juni 12, ikishirikisha wasanii mbalimbali nyota akiwamo yeye Nisha na nimeiongoza mwenyewe, kadhalika tupo katika mipangpo ya mwisho ya kuja kuitoa hadharani filamu mpya ya Kajala Masanja, kazi yake inaitwa Laana na ni bonge la filamu, ambayo shabiki hapaswi kuikosa," alisema Lamata.
Lamata, mmoja wa waongozaji mahiri nchini kwa sasa anatamba mtaani na kazi kadhaa kama Elimu Mtaani aliyotunga na kuiangdikia muswada, Jicho Langu na nyingine akizidi kuwakimbiza waongozaji wa kiume waliokuwa wametawala soko la filamu Tanzania.
Katika fikamu za Zena na Betina, Nisha ameigiza pamoja na Ulimboka Mwakilasa 'Senga' na Hanifa Daud 'Jenifer' na wakali wengine. Siyo ya kukosa hii kitu

No comments:

Post a Comment