STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, March 25, 2014

Kalapina atoa mpya kiulayaulaya

Karama Masoud 'Kalapina' akionyesha manjonjo yake jukwaani
NYOTA wa muziki wa Hip Hip nchini, Karama Masoud 'Kalapina' amefyatua 'single' mpya  iitwayo 'Hip Hop is Alive' aliomshirikisha msanii  'Q Chilla' ambayo anatarajia kuuachia rasmi kesho.
Akizungumza na MICHARAZO, Kalapina anayetoka kundi la Kikosi cha Mizinga alisema wimbo huo umerekodiwa katika studio za Rubby Records chini ya mtayarishaji wake Jallaman.
Kalapina alisema tofauti na alivyozoeleka kuimba hip hip ngumu, safari hii amekuja kivingine akiimba hip hip laini inayoweka kuchezeka akiwa amelenga soko la kimataifa zaidi.
"Huu ni ujio mpya wa Kalapina, nimelenga soko la kimataifa kwa kuimba wimbo huo kwa staili ya Ulaya na sijaegemea Marekani au Nigeria kama ilivyo kimbilio la wasanii wengi kwa sasa, na nitaachia hadharani kuanzia kesho Jumatano," alisema.
Kalapina alisema ameamua kubadilika kidogo ili kufanya muziki wake usikilizwe na watu wa rika lote na kuweza kuwarusha wasikilizaji wake na lengo lake kubwa ni kutaka kufungua soko la muziki wake anga la kimataifa badala ya kukomalia nyumbani tu.

No comments:

Post a Comment