STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, March 25, 2014

Easy Man kuweka Mashetani wake videoni

Easy Man  katika 'kichupa' chake cha Kasoro Wewe
MSANII anayetajwa kama 'mfalme' wa mchiriku nchini kwa sasa, Is'haka Salehe 'Easy Man',  anatarajiwa kurekodi video ya wimbo wake mpya uitwao 'Mashetani'.
Easy Man alisema wimbo huo ambao ni wa pili kwake baada ya kutesa na 'Kasoro Wewe', alisema kazi ya kurekodi video hiyo inatarajiwa kuanza keshokutwa chini ya kampuni moja iliyopo maeneo ya Temeke.
"Kuanzia Alhamisi natarajia kuanza kazi ya kurekodi video ya wimbo wangu wa 'Mashetani' na baada ya hapo nitaingia tena studio kwa ajili ya kurekodi wimbo mwingine ambao nitauachia kabla ya Mei mwaka huu," alisema Easy Man.
Msanii huyo alisema ana imani video ya wimbo wake wa 'Mashetani' unafunika kama ule wa 'Kasoro Wewe', huku akikatishwa tamaa baada ya kushindwa kuingia kwenye kinyang'anyiro cha Tuzo za Muziki wa Kili Music alizokuwa akiziombea awemo safari hii.

No comments:

Post a Comment