STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, March 25, 2014

Japanese ataka wasanii wa kike kujifunza kupiga ala

Japanese (kulia) akiwa na wanamuziki wenzake wa Jambo Survivors
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgxe5Rtm0ti7byoMQu71Qu2RCeP9KEud2GUkrLmeGrxVLRPJp1gKactUXZTOHXJoo7jhXXQbSZTnLG8klbNhVehA7oIbPN1esGX21SAjpyExhcK1wLO_mtK85shSRI2zmvGELH-iAE88iw/s1600/FIL0.JPG
Marehemu Asia Daruwesh enzi za uhai wake akionyesha umahiri wake katika kinanda
MUIMBAJI nyota wa zamani wa African Revolution na Double M Sound, Amina Ngaluma 'Japanese' amewataka wasanii wenzake wa kike kujibidiisha kujifunza kupiga ala za muziki badala ya kuishia kuimba tu.
Japanese alisema wasanii wengi wa kike wamekuwa wakikwepa kujifunza kupiga ala au kujifunza vitu zaidi ya uuimbaji na kuwafanya waachwe nyuma na wasanii wa kiume.
Alisema imefika wakati wanawake wenzake kuacha uvivu na badala yake kukamilia ala mbalimbali ili wawe wanamuziki kamili na kuweza kusimama pamoja na wanamuziki wa kiume wanaoonekana kutawala anga la muziki nchini.
"Mimi natunga, napanga muziki, napiga gitaa na ala nyingine, kitu ambachio natamani wasanii wa kike wengine wafuate nyayo ili kuondoa dhana muziki ni wa wanaume tu na sisi kazi yetu kuimba tena wakati mwingine kuitikia tu," alisema.
Alisema pia angependa kuona idadi ya wiambaji wa kike nchini inaongezeka maradufu kama ilivyokuwa miaka ya 1980-2000 waimbaji wa kike walipokuwa wengi na wengine kama marehemu Asia Daruwesh akiwa mahiri katika kupapasa kinanda kwa ustadi mkubwa.

No comments:

Post a Comment