STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 26, 2014

Mashetani Wekundu wafa tena, Arsenal yabanwa Everton yapeta

Edin Dzeko
Edin Dzeko akiwatungua Manchester United
Wilfried Bony
Hekaheka langoni mwa Arsenal

Everton's Ross Barkley
Shhhhh!
  JAHAZI la Manchester United limezidi kuzama baada ya usiku wa kuamkia leo kukandikwa mabao 3-0 kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Old Trafford na mahasimu wao wa jiji la Manchester, Manchester City.
Mabao ya Edin Dzeko aliyefunga mawili katika sekundu chache baada ya kuanza kwa mchezo huo na jingine la dakika 26 na lile la Yaya Toure dakika za 'jioni' yaliwafanya vijana wa David Moyes kushindwa kujua wamekumbwa na nini msimu huu.
Ushindi huo umeipeleka City hadi nafasi ya pili ikiiengua Liverpool itakayoshuka dimbani leo kuumana na Sunderland, kutokana na kufikisha pointi 66 baada ya kucheza mechi 29, mechi mbili pungufu na vinara wa ligi hiyo Chelsea wanaoongoza wakiwa na pointi 69.
Katika mechi nyingine, Arsenal ikiwa nyumbani ilinyang'anywa tonge mdomoni baada ya kulazimishwa sare ya 2-2 na Swansea City kwenye uwanja wa Emirates.
Wageni walitangulia kupata bao dakika ya 11 kupitia kwa Wilfried Bony kabla ya wenyeji kuja kusawazisha katika kipindi cha pili kupitia kwa Lucas Podolski katika dakika ya 73 na kuongeza jingine kupitia kwa Olivier Giroud.
Hata hivyo wakati Arsenal ikijiandaa kushangilia ushindi mchezaji wake Mathieu Flamini alijifunga katika harakati za kuokoa shambulizi langoni mwake na kuwapa sare Swansea na kugawa pointi moja moja.
Nao Everton wakiwa ugenini waliwaduwaza wenyeji wao Newcastle Utd kwa kuwakandika mabao 3-0, mabao yaliyowekwa kimiani na Barkley, Lukaku na Osman.
Kwa ushindi huo umeifanya Everton kufikisha pointi 57 na kupanda nafasi ya tano na kuishusha Tottenham Hotspur yenye pointi 56 ambayo inarudi katika nafasi ya sita.
Kivumbi cha ligi hiyo kitaendelea tena usiku wa leo kwa michezo miwili, Liverpool itakayoumana na Sunderland na West Ham Utd itaikaribisha Hull City.

No comments:

Post a Comment