STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 20, 2013

Zola D awashukuru Watz msiba wa Ngwair, Langa, lakini...!


Mwili wa Ngwair ukiingizwa kaburini, ambapo Zola D (mwenye miwani) naye alikuwa mmoja wa walioshiriki mazishi hayo mjini Morogoro.

BARUA MAALUM KUTOKA KWA DAVID MICHAEL MLOPE,ZOLA D KWENDA KWA WATANZANIA WOTE WALIOSHIRIKI KATIKA MSIBA WA MANGWEAR...

DAVID MICHAEL MLOPE BOX 70098 DAR ES LAAM TANZANIA.
PHONE +255715296889.

habari za leo watanzania wote ,nachukua nafasi hii kwa niaba ya wasanii wa kundi la chemba sqward east zoo,kuwashukuru watanzania wote walioshiriki katika msiba wa ndugu yetu mpendwa mangwear hakika nimeona upendo wenu kwa kumzika ndugu yetu Arbert k mangwear kwa upendo wenu mkubwa sana,mimi binafsi sina cha kuwalipa ila nina imani kubwa sana Mungu atawalipa,na sio kwa mangwear tu naomba mzidi kushilikiana na sisi wasanii wenu hata siku nikifa mimi au msanii mwingine naomba mtuzike KWA UPENDO msituache maana sie sote ni binadamu tunapita tu hapa kwenye hii dunia kila mtu atakufa muhimu ni kupendana na kushirikiana kwa upendo,pia kama tunagombana hapa duniani ni bora tupatane kabla ya kifo kutukumba siku yetu ya kufa hakuna anaetambua itakuwa lini, maana Mungu alisema ukisamehe na yeye atakusamehe siku yako ya kihama,kuna mambo mengi nimejifunza kwenye hii dunia,kwamba tujitahidi kufanya yaliyo mema kutengeneza njia bora siku tukifa,napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru sana wana kamati wote waliojitolea tokea mwanzo kuandaa safari kutoka south africa mpaka tanzania asante sana BRO P FUNK MAjANI , BONGO RECORDS kwa upendo wako na mchango wako kwetu sie wadogo zako Mungu ATAKULIPA ZAIDI NA ZAIDI ,ASANTE SANA RADIO CLOUDS FM KWA KUSHIRIKI KWA UPENDO WENU MKUBWA ,na wafanyakazi wake wote walioshiriki kwa upendo katika kukamilisha safari ya mpendwa wetu MANGWEAR,asante sana BRO ADAMU jUMA VISUAL LAB NIMEONA KAZI KUBWA ULIYOIFANYA MUNGU AKUBARIKI SANA ENDELEA KUWA NA MOYO HUO HUO , ASANTE SANA, BRO MIRAD AYO,BRO MAjIZO,BRO TC TIMOTH CHERULA,ADAMU MCHOMVU,RADIO TIMES FM,RADIO EAST AFRICA NA EAST AFRICA TV,ITV,CHANEL TEN BRO RIZ 1 KIKWETE,BRO SUGU,SIST j DEE,Dj CHOKA, PUSH NA WENGINE WENGI,AMBAO NIMEWASAHAU MAjINA YENU ASANTENI SANA SANA WOTE WALIOTOA MAGARI YAO KWENDA MOROGORO KUZIKA,PIA ASANTE SANA WANAKAMATI WA MOROGORO,ASANTE SANA VIONGOZI WA POLICE DAR ES SALAAM NA VIONGOZI WA POLICE MOROGORO KWA KUIMALISHA ULINZI KATIKA MSAFARA WA MANGWEAR KUANZIA DAR MPAKA MOROGORO NINA MAMBO MENGI SANA YA KUANDIKA ILA NAONA KWA LEO NISHIE HAPA,NACHUKUA NAFASI HII KUAMBIA NAWAPENDA SANA WATANZANIA WENZANGU PIA NAWAPENDA VIONGOZI WANGU WA TANZANIA PIA NAIPENDA NCHI YANGU YA TANZANIA NIPO TAYARI KUFA KUITETEA NCHI YANGU NA WANACHI WANGU NAWATAKIA MAISHA MEMA NA FAMILIA ZENU NI MIMI MTIIFU WENU KATIKA UjENZI WA TAIFA LETU TUKUFU, DAVID MICHAEL MLOPE AKA ZOLA D.ITAENDELEA!!!!!

No comments:

Post a Comment