STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 20, 2013

Waraka namba 2 wa Zola D kwa Watanzania

Zola D katika pozi
BARUA MAALUM KUTOKA KWA DAVID MICHAEL MLOPE,aka ZOLA D KWENDA KWA WATANZANIA WOTE WALIOSHIRIKI KATIKA MSIBA WA MANGWEAR.pamoJa na LANGA KILEO.

DAVID MICHAEL MLOPE BOX 70098 DAR ES LAAM TANZANIA.
PHONE +255715296889.
barua no 2.

naendelea pale nilipoishia kwenye barua ya mwanzo namba 1 ...... habari zenu ndugu zangu watanzania hope wote ni wazima na mnaendelea na mishe za maisha mimi mzima siJambo Japo nina stress nyingi sana mpaka nimepungua kg 3,kutokana na mawazo na kuto kulala tokea msiba wa arbert mangwear pia tumepata pigo Jingine la mdogo wetu langa kileo,siJui niseme nini kwa Jinsi inavyo niuma ila nina mwachia Mungu maana ndio kazi yake pia pole sana wazazi wa langa kileo baba na mama pamoJa na familia yote kwa uJumla pia asante sana watanzania wote walioJitokeza kwenye safari ya kumsindikiza ndugu yetu msanii mwenzetu langa kileo leo nataka kugusia sana upande wa maisha yetu na dini kama binadamu tunaopita tu kwenye hii dunia maana kila mtu atakufa vitabu vya dini vimeandika.Ndugu zangu wapendwa watanzania dunia imekwisha ndugu zangu tuanze kufanya ibada na kutenda yaliyo mema coz free masons wanawatumia ndugu zetu kwenye big brother na seemu mbali mbali kuwaonyesha wakiwa watupu uchi na kuwadanganya kwa pesa,na sasa wameingia africa mashariki kwa kishindo sana hawa free masons Juzi tu nimepigiwa simu na watu kampuni Jina siri yangu wanataka nikacheze video ya ngono na mwanamke kwa kitita cha milion 70 nikawaeleza siwezi kufanya uchafu kama huo,na leo tena wamenipigia wakisema watanipa milion 100 bado nimekataa Je unaelewa kwa nini nimekataa? free masons wanataka viJana shupavu na wenye akili na vipaJi ili waweze kuwatumia kuitangaza dini yao na wanaweza kukupa maisha ya Juu kwa gharama yoyote ile, Mungu atuepushe nao na Mungu atulindie watoto wetu inshallah wasiingie kwenye dini ya kishetani,wahi kuwapeleka madrasa watoto mapema waitambue dini mapema na kuwapeleka kwenye mafunzo ya dini kwenye makanisa tuliyoyazoea tokea kitambo na tuachane na makanisa mapya yanayoanzishwa kila kukicha na wachungaJi wao wanaJiita miungu watu,ndugu zangu naelewa watu wanaweza kuniona kama nilie changanyikiwa hapana ila nimeamua kupoteza muda wangu kukaa chini na kuandika machache ninayoyaona kwa upeo wangu na vipaJi alivyonipa Mungu kuelimisha na kuburudisha,siwezi kukaa kimya pale ninapo tizama taifa langu lina teketea kwa maovu,na tunapelekeshwa kishetani na dini feki na makampuni ya kigeni katika nchi yetu tuna acha utamaduni wetu na tunaingia kwenye utamaduni wa watu wa kishetani kwa upeo wetu mdogo na umasikini tumetekwa na pesa na starehe kiasi kama sisi wasanii ukitizama storia ya msanii mwanzo kabla aJawa super star alikuwa ni mtu wa kufanya ibada ila sasa amekuwa super star awezi tena kufanya ibada wala kutoa dhaka au kuwasaidia wazazi wake kisa yeye ni star na yupo bussy Je swali huyu star msanii ni kioo cha Jamii au amegeuka kuwa moto wa Jamii? kila kukicha kwenye magazeti utaskia story za sifa mbaya na picha chafu za wasanii sehemu flani wakifanya ngono na mambo mengine ya kumchafua Mungu wetu,ndugu zangu wasanii naomba tubadilike na tuwe mfano ili tuweze kuliongoza taifa letu salama na tuwafundishe wadogo zetu waige mfano mzuri wa tabia zetu nJema na sio uchafu wetu,ndugu zangu watanzania mimi sitaki kuwachosha maana nina MAMBO MENGI SANA YA KUANDIKA ILA NAONA KWA LEO NISHIE HAPA,NACHUKUA NAFASI HII KUAMBIA NAWAPENDA SANA WATANZANIA WENZANGU PIA NAWAPENDA VIONGOZI WANGU WA TANZANIA PIA NAIPENDA NCHI YANGU YA TANZANIA NIPO TAYARI KUFA KUITETEA NCHI YANGU NA WANACHI WANGU NAWATAKIA MAISHA MEMA NA FAMILIA ZENU NI MIMI MTIIFU WENU KATIKA UjENZI WA TAIFA LETU TUKUFU, DAVID MICHAEL MLOPE AKA ZOLA D.ITAENDELEA!!!!!

No comments:

Post a Comment