STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, October 6, 2014

Kassim Selembe achekelea kunolewa na Rishard Adolph

KIUNGO mshambuliaji mpya wa Polisi Moro, Kassim Suleiman 'Selembe' amesema anajisikia faraja kubwa kufanya kazi chini ya nyota wa zamani wa kimataifa wa Tanzania Mohammed Rishard 'Adolph'.
Aidha mchezaji huyo aliyekuwa akiichezea Coastal Union, alisema kusuasusa kwa Polisi kwa sasa kunatokana na 'ugeni' wao wa Ligi Kuu, ila kadri watakavyokuwa wakiizoea watawashangaza watu.
Akizungumza na MICHARAZO, Selembe, alisema anajisikia furaha kufanya kazi na kocha Adolph, nyota wa zamani wa Yanga, Pan Africans na Taifa Stars ikizingatiwa ni moja wa nyota wa Tanzania waliojijengea jina kubwa Afrika.
"Kwa mchezaji yeyote anayejitambua kufanya kazi na mtu kama Adolph ni fahari kwa sababu alijijengea jina kubwa ndani na nje ya Tanzania enzi za uchezaji wake, wachezaji tunamfurahia," alisema.
Kiungo wa zamani wa Azam alisema kocha Adolph ni bonge la kocha na anawafanya wachezaji wa Polisi kujiamini na kurejea Ligi Kuu kabla ya yeye kuungana nao akitokea Coastal Union.
Juu ya mwenendo wa kikosi chao, Selembe alisema wanazidi kuimarika kadri wanavyoizoea ligi na kwamba hawana hofu ya kurejea walikotoka akidai ni mapema mno kujadili jambo hilo.
Timu hiyo ilipanda daraja sambamba na Ndanda na Stand United na ilianza kwa kufungwa mechi moja na kuambulia sare mbili katika mechi zao tatu za awali ya ligi hiyo inayoenda mapumziko.
Ligi hiyo itakuwa likizoni kwa wiki moja kupisha mchezo ya kimataifa ya kirafiki unaotambuliwa FIFA Taifa Stars itakapovaana na Benin na itaendelea tena kuanzia Oktoba 18.

No comments:

Post a Comment