STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 7, 2014

Wasanii wahimiza kuhudhuria semina ya Haki Miliki

Kama wanavyopeana sapoti kwenye tuzo wasanii wanapaswa pia kuhudhuria semina mbalimbali kupata uelewa na wa mambo yanayowakwaza
Na Kipimo Abdallah
UMOJA wa Mashirikisho ya Sanaa Tanzania umewaomba wasanii nchini kujitokeza katika semina ambayo inatarajia kufanyaka Oktoba mwaka huu katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Umoja huo Godfrey Ndimbo wakati akizunumza na waandishi wa habari  jijini Dar es Salaam.
Alisema umoja wao unatoa pongezi kwa taasisi hiyo ya Haki Neel Production Company ambayo imetambua msanii wa Tanzania.
Ndimbo alisema semina hiyo itajikita katika kuwaelimisha wasanii kuhusu mafao ya uzeeni, matibabu kupitia bima ya afya, Haki Miliki, Haki Shiriki na Kodi.
“Napenda kuwaomba wasanii wa Tanzania kujitokeza kwa wingi katika semina hiyo kwani itawajengea uwezo mzuri katika kutambua haki zao nyingi ambazo zinakiukwa, ” alisema.
Ndimbo alisema katika semina hiyo wanatarajia kuwahusisha watumishi kutoka taasisi mbalimbali kama Poilisi, Uhamiaji na Mahakimu.
Katibu Mkuu huyo alisema lengo la kushirikisha sekta hizo ni kuhakikisha kuwa wanakuwa na ufahamu dhidi ya kazi hizo za wasanii nchini ili wajione kuwa wana haki ya kutetea kazi hizo.
Alisema lengo ni kuhakikisha kuwa sheria inayotumika kutoa hukumu kwa husika inakuwa na tija kwani kwa sasa ni ndogo jambo ambalo linakwamisha maendele ya tasnia hiyo.
Katibu Mkuu huyo alisema pia wanawakaribisha waandishi wa habari katika semina hiyo ili kuhakikisha kuwa wanakuwa na ufahamu mzuri wa kutosha kuhusiana na tasnia hiyo.
Alitoa wito kwa wadau wengine kujitokeza kwa wingi ili kusaidia na taasisi ya Haak Neel Production Company ambayo imeonyesha jitihada za kutambua nafasi ya msanii.
mwisho

No comments:

Post a Comment