STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 7, 2014

Newz Alert! Mwanasheria Mkuu ZNZ afutwa kazi

HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,Othman Masoud amefutwa kazi na Rais wa Zanzibar, Dk Mohammed Ali Shein.
Taarifa kutoka visiwani humo zinasema kuwa Mwanasheria huyo aliyeamua kutumia demokrasia yake katika Bunge la Katiba kwa kupigia kura za ndiyo na hapana vipengele na ibara za Rasimu ya Katiba Mpya amefutwa kazi usiku huu.
Inaelezwa maamuzi hayo ya Dk Shein yamekuja ikiwa imesalia saa chache kabla ya rasimu huyo kukabidhiwa kwa viongozi wakuu wa nchi kesho mjini Dodoma na nafasi yake imeelezwa inazibwa na aliyekuwa Mwansheria Mkuu Msaidizi, Said Hassan Said.
hata hivyo haikuelezwa sababu ya kufutwa kazi kwa Mwanasheria huyo ambaye kwa baadhi ya wajumbe na wananchi wa visiwani humo wanamuona kama 'Msaliti' kwa alichokifanya kwenye Bunge Katiba lililomalizika hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment