STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 7, 2014

Baby Madaha 'ala shavu' Ujerumani

STAA wa 'Amore' na 'Summer Holliday', Baby Madaha amekula shavu baada ya kuteuliwa kwenda kushiriki filamu ya kimataifa nchini Ujerumani iitwayo 'Saint & Ghost'.
Muigizaji huyo aliliambia MICHARAZO kuwa, anajiandaa kupaa kwenda Ujerumani kushiriki filamu hiyo itakayotengenezwa na mtayarishaji maarufu Dittiman.
Baby Madaha alisema filamu hiyo itawashirikisha pia waigizaji wengine kutoka nchini Ujerumani na kutamba ni nafasi yake ya kujitangaza zaidi kimataifa.
"Nashukuru Mungu nimepata bahati ya kuteuliwa kwenda kushiriki katika filamu inayotengenezwa na Prodyuza Dittiman iitwayo 'Saint and Ghost' kazi hiyo itafanyika nchini Ujerumani," alisema Baby Madaha.
Msanii huyo anayepanda farasi wawili kwa wakati mmoja kwa maana ya kuimba muziki na kucheza filamu, alisema uteuzi wake umekuja baada ya kuwavutia waratibu wa filamu hiyo kupitia kazi mbalimbali alizocheza ambazo zimekuwa zikifanya vyema kimataifa.
Baadhi ya filamu alizocheza mwanadada huyo ni 'Desperado', 'Ray of Hope', 'The Gal Bladder', 'The Lost' na 'House No. 44'.

No comments:

Post a Comment