STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 7, 2014

Baby J kutanguliza Katapila lake videoni

http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2014/01/baby-J.jpg
NYOTA wa muziki wa kizazi kipya kutoka visiwani Zanzibar, Jamila Abdullah 'Baby J' amesema ameamua kubadili mawazo ya kuachia 'audio' ya 'Katapila' na badala yake ataanza na video.
Akizungumza na MICHARAZO, Baby J alisema ameamua kutoa video kabla ya 'audio' kwa nia ya kuwapa ladha tofauti mashabiki wake.
Baby J alisema video hiyo inayoendelea kurekodiwa na kampuni ya Visual Lab (Next Level) chini ya mtaalam Adam Juma na ataiachia hewani mara baada ya kukamilika kurekodiwa.
"Badala ya kuanza kuachia 'audio' ya 'Katapila' nimeamua nitoe kwanza video ambayo inaendelea kutengenezwa na Adam Juma,' alisema Baby J.
Wimbo huo mpya unaokuja baada ya 'Nimempenda Mwenyewe' kufanya vema hewani, umetengenezwa na maprodyuza wawili tofauti, Shirko na Lil Ghetto.

No comments:

Post a Comment