STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 7, 2014

Mkude, Mgeveke waongezwa Stars


http://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2014/05/IMG_7000.jpgKATIKA kuhakikisha wanapata ushindi katika mechi yao ya Jumapili dhidi ya Benin, Kocha Mart Nooij ameongeza wachezaji watatu kwenye kikosi cha Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ili kukiongezea nguvu.
Taifa Stars inajianda kukabiliana na Benin katika mechi ya Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA)  itakayofanyika Jumapili (Oktoba 12 mwaka huu) jijini Dar es Salaam.
Wachezaji walioongezwa ni kiungo Jonas Mkude na mlinzi Joram Mgeveke kutoka timu ya Simba, pamoja na mlinzi Gadiel Michael wa Azam.

No comments:

Post a Comment