STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 7, 2014

Ligi ikienda mapumziko, Yanga yapumua, Mtibwa Sugar inatisha

Yanga wanaenda mapumziko wakipumua nafasi ya tatu
Coastal Union bado wanajikongoja

Watetezi Azam wakiporomoka hadi nafasi ya pili wakiwapisha Mtibwa kuwaongoza
Mtibwa timu pekee iliyoshinda mechi zake 100%

Ruvu Shooting ndiyo ambayo haijafunga bao hata mmoja mpaka sasa. Ni kwamba pengo la Maguli (kushoto) halijapata mrithi wa kuliziba?
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgboM03iAUZPCYvuYadSX-DrgxLYiOqanpQRh7w9oQyCDx_BclL4a6oF2VrzSbdjwrhAhFHPKlzRnMprs771Eep9DtnpEeGeoC5KrCHMmrC1wfNHGwyf56QiZMMSUqM8AmM2gVywZA6S2I/s1600/HMB_8265.JPG
Simba wataivaa Yanga mechi ijayo ikiandamwa na mdudu wa sare
RAUNDI ya tatu ya Ligi Kuu Tanzania Bara umemalizika  mwishoni mwa wiki na kushuhudia jumla ya mabao 44 yakitinga wavuni, huku mshambuliaji wa Azam Didier Kavumbangu akiongoza kwa kupachika mabao manne kati ya hayo.
Kavumbagu aliyetua Azam akitokea Azam anafuatiwa kwa karibuni na Ally Shomari wa Mtibwa mwenye mabao matatu kiisha kufuatiwa na wachezaji wanne wenye mabao mawili kila mmoja.
Timu yenye fowadi kali mpaka sasa wakati lihi ikienda mapumziko kwa wiki moja ni Mtibwa Sugar na Ndanda FC zenye mabao sita kila moja, kisha kufuatiwa na Azam yenye mabao matano kisha Yanga na Simba zikafuatia zikiwa zimetumbukiza kimiani mabao manne kila moja.
Pamoja na kuwa kinara wa kufunga mabao Ndanda pia ndiyo timu yenye ukuta mwepesi ikiruhusu mabao sita mpaka sasa ikifuatiwa na timu za Stanmd United na Polisi waliopanda pamoja ligi ya msimu huu zikiwa zimeruhusu mabao matano.
Ruvu Shooting ndiyo timu iliyo na safu butu mpaka sasa ikiwa haijafunga bao lolotewakifuatiwa na Mbeya City, Mgambo na JKT Ruvu wenye bao moja moja.
Ukuta wa chuma wa ligi hiyo mpaka sasa ni ule wa klabu ya Mbeya City ambayo haujaruhusu bao lolote kwake huku Mtibwa Sugar na Azam zikifuata kwa kufungwa bao moja tu kila moja.
Yanga ambayo ilianza kwa kipigo katika ligi ya msimu huu imechupa toka maeneo ya kati hadi nafasi ya tatu wakiwaacha watani zao watakaoumana nao katika mechi yao ijayo wakiwa na pointi tatu wakishika nafasi ya 10.


MSIMAMO KAMILI WA LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                               P   W    D    L    F    A   GD   Pts

01. Mtibwa Sugar     03  03   00  00  06   01  +5   09
02. Azam                 03  02   01  00  05   01  +4   07
03.Yanga                  03  02   00  01  04   04  00   06
04. Mbeya City          03  01  02  00  01   00  +1   05
05.Kagera Sugar       03  01  01   01  03   02 +1   04
06. Prisons                03  01  01   01  03  02  +1  04
07.Coastal Union       03  01  01   01  04  04   00  04
08.Stand Utd             03  01  01   01  03   05  -2   04
09. Ndanda Fc           03  01  00   02  06    06  00  03
10.Simba                  03  00  03   00  04    04  00  03
11. Mgambo JKT       03  01  00   02   01    02  -1  03
12. Polisi Moro          03  00   02  01   03    05   -2  02
13.JKT Ruvu             03  00   01  02   01   04   -3  01
14. Ruvu Shooting     03  00  01   02  00   04   -4  01

http://static.goal.com/462500/462526_heroa.jpg
Didier Kavumbangu  (kushoto) akipongezwa na wenzake
Wafungaji Bora:
4- Didier Kavumbagu(Azam)


3-
Ally Shomari (Mtibwa)


2-
Shaaban Kisiga (Simba), Nassor Kapama (Ndanda), Ame Ally (Mtibwa), Rashind Mandawa (Kagera)


1- Emmanuel Okwi, Amissi Tambwe (Simba), Coutinho, Kelvin Yondan, Haruna Niyonzima, Simon Msuva (Yanga), Deo Julius (Mbeya City), Danny Mrwanda, Nicolaus Kabipe, Bakari (Polisi-Moro),  Salum Kanoni,  (Kagera), Aggrey Morris  (Azam), Ernest Joseph, Paul Ngalema, (Ndanda), Jacob Mwaitalako, Ibrahim Kihaka, Laurian Mpalile (Prisons), Lutimba Yayo, Rama Salimu, Joseph Mahundi, Hussein Sued, (Coastal), Ramadhani Pella (Mgambo), Mussa Mgosi (Mtibwa), Jabir Aziz (JKT Ruvu), Salum Kamana, Heri Mohammed, Mussa Said(Stand Utd)

No comments:

Post a Comment