STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 7, 2014

Hammer Q kuweka kibakuli chake videoni

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjPuXhtoeR4zztOCIdP7ZAekZVHi6Yl2h8tpe5fFNe4ECtPzhUsg7Z-Na338MBN_tvxM5xrs2kGZ0v9Fn6DnsJSOz75hXNxqqYAL7QbNtlUvMB7tp7ZN4t-71MOswqFm3nnUcz3wFF5r6g/s1600/Hammer+Q.jpgMUIMBAJI mahiri wa muziki wa taarab, Hammer Q ameachiwa wimbo wake binafsi uitwao 'Kibakuli', ambao anajipanga kuutengenezea video yake mapema hivi karibuni.
Hammer Q aliyewahi kutamba kwenye muziki wa kizazi kipya na wimbo wa 'Lady' kabla ya kuhamia kwenye taarab, ameachiwa wimbo huo uliopo kwenye mduara.
Wimbo huo umetengenezwa na mtayarishaji aitwae Anta Nation na  umeanza kutamba kwenye redio na mitandao ya kijamii.
Msanii huyo amesema kwa sasa anafanya mchakato ili kutengeneza video ya wimbo huo mapema kuwapa burudani zaidi mashabiki wake.
Hammer Q mbali na kufanya muziki kama 'solo artist' pia analiimbia kundi maarufu na miondoko ya mduara ya Zanzibar la Offside Trick sambamba na kufanya kazi na mkewe Salha Abdallah 'Salha wa Hammer'

No comments:

Post a Comment