STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, October 6, 2014

Ronaldo azidi kutesa La Liga, Messi abakisha 2 tu!

Cristiano Ronaldo
Ronaldo akishangilia moja ya mabao yake matatu usiku wa jana
Lionel Messi of Barcelona
Messi akifunga bao lake la 349 katika La liga dhidi ya Rayo Valecano
WAKATI Lionel Messi akiwa amesaliwa na mabao mawili tu ili kufikia rekodi ya mabao katika Ligi Kuu ya Hispania, mpinzani wake Cristiano Ronaldo usiku wa jana alifunga hat-trick yake ya 22 wakati akiisaidia Real Madrid kushinda nyumbani kwa mabao 5-0 dhidi ya Athletic Bilbao.
Ronaldo alifunga mabao hayo katika dakika za 2, 55 na 88 akisaidiwa na Gareth Bale na Pepe, huku mabao mengine yakiwekwa kimiani na Karim Benzema katika dakika za 41 na 69 na kuifanya Madrid kufikisha jumla ya pointi 15, nne nyuma ya vinara Barcelona ambao wameendelea kushinda mfululizo katika ligi hiyo.
Mabao hayo yamemfanya Ronaldo kufikia rekodi ya ha trick nyingi za gwiji wa Madrid Alfredo de Stephano na Telmo Zarra waliowahi kufunga pia hat trick 22 akimtangulia Messi mwenye ha trick 19 akikamata nafasi ya tano.
Hata hivyo Messi aliisaidia Barcelona kushinda mechi yao ya sita na kuweka rekodi ya kutoruhusu kufungwa bao lolote katika mechi saba mfululizo wakati wakiizamisha Rayo Valecano kwao kwa mabao 2-0.
Messi alifunga bao lililomfanya afikishe jumla ya mabao 349 katika La Liga na kushika nafasi ya pili nyuma ya  gwiji wa zamani wa Athletic Bilbao, Telmo Zarra aliyetamba miaka ya 1940-50 aliyefunga mabao 351, ikiwa na maana akifunga mabao mawili tu atamfikia na kuifukizia rekodi mpya katika ligi hiyo maarufu.
Bao jingine la wababe hao wa Nou Camp liliwekwa kimiani na Neymar na kuwafanya wachezaji hao wawili wanaotoka mataifa hasimu katika soka Amerika ya Kusini, Argentina na Brazil kufikisha jumla ya mabao 13 wakicheza pamoja..
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Atletico Madrid iokiwa ugenini ilikumbana na kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Valencia, huku Cordoba na Getafe walitoka sare ya 1-1 na Eibar kulazimishwa sare ya mabao 3-3 na Levante.
Almeria na Elche zilitoshana nguvu kwa sare ya 2-2 na Malaga ikaifumua 2-1 Grenada waliwafuata nyumbani kwao, huku Sevilla ikipata ushindi mnono nyumbani dhidi ya Deportivo la Coruna waliowafumua mabao 4-1 na Celta Viro ililala nyumbani 3-1 kwa Villarreal na Espaniol ilitaka nyumbani kwa kuilaza Real Sociedad kwa mabao 2-0.
ANGALIA WAKALI WA HAT TRICK LA LIGA
Cristiano Ronaldo 22
Alfredo Di Stefano 22
Telmo Zarra 22
Edmundo Suarez 19
Lionel Messi 19
Barcelona's Lionel Messi and Neymar
Neymar na Messi wakishangilia mabao yao wakati wakishinda ugenini na timu iliyopoteza wachezaji wao wawili uwanjani kw akandi nyekundu Rayo Valecano.






























































No comments:

Post a Comment