STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 10, 2014

Kocha Marsh asubiri vipimo vya mwisho kuanza matibabu

Kocha Msaidizi wa Taifa Stars, Sylvester Marsh (Pichani kushoto) ambaye amelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) anasubiri vipimo vya mwisho ili aweze kuanza matibabu.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemtoa kocha huyo nyumbani kwake jijini Mwanza na kumleta Dar es Salaam kwa lengo la kuhakikisha anapata matibabu zaidi na kwa uangalizi wa karibu.
Tayari majibu ya kipimo cha kwanza yameshapatikana, hivyo yanasubiriwa majibu ya kipimo kingine ili aweze kuanza rasmi matibabu, lengo likiwa ni kubaini kitaalamu ugonjwa unaomsumbua.

No comments:

Post a Comment