STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 10, 2014

Abdallah Juma aililia TFF, alia na Nkongo

Abdallah Juma enzi akiwa Simba
MSHAMBULIAJI nyota wa Mtibwa Sugar, Abdallah Juma ameliomba Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuwafuatilia kwa ukaribu marefa wanaochezesha Ligi Kuu ili kuepusha 'maafa' yanayoweza kutoka uwanjani kutokana na maamuzi yao mabovu na yenye upendeleo.
Pia ameliomba shirikisho hilo kuweka chini ya uangalizi uwanja wa Sokoine-Mbeya ambao kwa msimu huu umekuwa ukilalamikiwa na baadhi ya klabu kukithiri kwa vitendo vya hujuma kwa timu wageni.
Mshambuliaji huyo pekee mzawa aliyefunga hat-trick kati ya tatu zilizofungwa msimu huu, alisema waamuzi wamekuwa wakifanya maamuzi mabovu yanayowatia hasira wachezaji na mashabiki.
Mchezaji huyo alisema ni vyema TFF wakawa wanafuatilia waamuzi hasa kwenye mechi hizi za duru la pili ambalo klabu huwa zikitafuta nafasi za kuwania ubingwa na kuepuka kushuka daraja.
"Mimi huwa siyo mlalamishi kwa waamuzi, lakini tulichofanywa jana kwenye uwanja wa Sokoine kwa kunyimwa mabao mawili ya wazi moja nikilifunga mimi kwa shuti kali la mbali inaumiza," alisema.
Alisema mbaya alienda kumuuliza mwamuzi, Israel Nkongo sababu ya kulikataa bao lake lililokuwa la kusawazisha na kuishi kutupiwa maneno machafu na kejeli.
"Sidhani kama huyu mwamuzi anastahili kuendelea kuchezesha ligi kwa alichokifanya kwetu na hasa kwangu kwa kunitusi baada ya kwenda kumuuliza," alisema mshambuliaji huyo wa zamani wa Simba.
Strika huyo alisema mbali na TFF kuwafuatilia kwa makini waamuzi walioteuliwa kuchgeza mechi za lala salama za ligi hiyo, pia waumulike uwanja wa Sokoine kwa kukithiri vitendo vya uzalendo.
"Majuzi wenzetu wa Ruvu Shooting walifanyiwa vitendo kama hivyo, jana tumefanyiwa sisi na hata Yanga, Ashanti walishakuja hapa na kulalamika, ni vyema TFF wakaufuiatilia uwanja huu," alisema.
Juma alisema kunyamazia vitendo vya kizalendo siyo tu vinatrudisha nyuma soka, lakini pia vinahatarisha usalama na amani uwanjani kwa sababu zipi timu ambazo mashabiki wao siyo wavumilivu.
"Fikiria jana tu imetokea rasbha kubwa uwanjani baada ya mechi kwa kuharibiwa kwa viti sababu ya maamuzi ya upendeleo yaliyofanywa je kwa mashabiki wahuni hali inakuwaje," alihoji mchezaji huyo wa zamani wa AFC Arusha.
Mtibwa Sugar ilikuwa uwanja wa Sokoine kuumana na Mbeya City na kulazwa mabao 2-1, huku viongozi wake wakilalamika kunyimwa mabao mawili ya wazi na mwamuzi Nkongo ambaye MICHARAZO halikufanikiwa kumpata kujibu tuhuma alizotupiwa na Juma.

No comments:

Post a Comment