STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, February 11, 2014

Wachezaji Simba kuwekwa kitimoto Msimbazi

Simba ikiwa na makocha wake, Logarusic (kulia) na Matola (kushoto waliosimama)
Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage anayetkutana na wachezaji leo mchana klabuni kwao
MWENYEKITI wa klabu ya Soka ya Simba, Ismail Aden Rage mchana wa leo anatarajia kukutana na kuzungumza na wachezaji ili kujua kinachoendelea baina yao na benchi lao ufundi baada ya kuelezwa kuna 'mgomo' baridi uliosababisha Simba kupata matokeo mabaya katika mechi zao mbili zilizopita.
Hata hivyo uongozi wa Simba umenukuliwa jana ukisema kikao hicho ni cha kawaida na hakina uhusiano wowote na matokeo ya mechi zilizopita ambapo Simba iliambulia pointi moja katia ya sita.
Awali MICHARAZO ilipenyezewa taarifa kuwa, wachezaji wa Simba watakutana na uongozi wa Simba leo saa 6 mchana ili kuwekwa kitimoto kama njia ya kuzima mgomo baridi uliowekwa na wachezaji dhidi ya kocha wao, Zdravko Lugarusic anayedaiwa amekuwa mkali na anatusi wachezaji wakati wa mazoezi.
"Matokeo ya Simba siyo yanatokana na timu kushuka kiwango, bali wachezaji wanamuonyeshea kocha wao ndiyo wanaoweza kumbeba au kumuangusha kwa vitendo vyake vya kuwafanya kama watoto wadogo kwa kuwatusi na kuwakaripia ovyo hata katika makosa yanayopaswa kuelezwa kwa upole," chanzo kilidokeza.
Hata hivyo Msemaji wa Simba, Asha Muhaji alinukuliwa jana na kituo kimoja cha redio akisema kikao hicho ni cha kawaida na kukanusha taarifa za kuwepo kwa mgomo baridi.
Kikao hicho kimeitishwa na Mwenyekiti Ismail Aden Rage na kitawahusisha wachezaji pekee yao kabla ya uongozi huo kukutana tena na benchi la ufundi, lengo likiwa kuweka mambo sawa kabla ya kuifuata Mbeya City watakaoumana nao katika mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara siku ya Jumamosi jijini Mbeya.
Simba ilianza mechi zake za ugenini kwa kulazimishwa sare ya 1-1 na Mtibwa Sugar, wakilazimika kurejesha bao kabla ya kulala Mkwakwani Tanga Jumapili walipoumana na Mgambo JKT iliyokuwa mkiani kwa msimamo kitu ambacho kimeishtua klabu hiyo kwa kuhisi mambo siyo mazuri.
Mabingwa hao wa zamani wa soka, kwa kipigo cha Mgambo wamerejeshwa hadi kwenye nafasi yao ya nne waliyokuwa awali kutokana na Mbeya City kuzinduka toka kwenye kipigo cha Yanga kwa kuilaza Mtibwa Sugar na kufikisha pointi 34 tatu zaidi ya ilizonazo Simba.
Katika mfululizo wa ligi hiyo kesho kwenye uwanja wa Chamazi, maafande ndugu, JKT Ruvu na Ruvu Shooting zinatarajiwa kupepetana kwenye pambano pekee.
Timu hizo zitakutana zikiwa zimetoka kupoteza mechi zao za mwisho,. JKT Ruvu ambao ni wenyeji wa mechi hiyo wakishtukizw ana kipigo cha Ashanti United na Ruvu Shooting kubabuliwa mabao 3-1 na Prisons Mbeya.

No comments:

Post a Comment