STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, February 11, 2014

Inspekta Harun 'Babu' Hujachelewa Bwana!

Babu akionyesha manjonjo yake jukwaani
MSANII mkongwe wa muziki wa kizazi kipya nchini, Haruna Kahena 'Inspekta Harun' .a.k,a Babu ameachia wimbo mpya uitwao 'Haujachelewa' ikiwa ni utambulisho wa albamu yake mpya atakayoizindua mwezi ujao.

Akizungumza na MICHARAZO, Inspekta Harun alisema wimbo huo ameurekodia kwa mtayarishaji Mbezi na ni kati ya nyimbo zitakazokuwa katika albamu mpya itakayofahamika kwa jina la 'Sharubu za Babu'.

Inspekta alisema tayari wimbo huo umeshaanza kusikika hewani tangu Ijumaa iliyopita na anashukuru umepokelewa vyema na mashabiki wa muziki nchini.

"Nimeachia wimbo wangu mpya uitwao 'Hujachelewa' chini ya prodyuza Mbezi ikiwa ni maandalizi ya albamu yangu iitwayo 'Sharubu za Babu'," alisema Inspekta Harun.

"Albamu hiyo mpya natarajia kuizindua mwezi ujao (Machi) pale Dar Live, taarifa zaidi juu ya wasanii watakaonisindikiza tutafahamisha kadri siku zinavyosonga mbele ila Babu nimerejea kwa kishindo," aliongeza msanii huyo.

Nyota huyo aliyewahi kutamba nchini na vibao murua kama 'Mtoto wa Geti Kali', 'Rapu Katuni', 'Simulizi la Ufasaha', 'Ngangari', 'Asali wa Moyo', 'Nje Ndani' na 'Tunajirusha' na nyingine.
===========================

No comments:

Post a Comment