STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, February 11, 2014

KIbao Kata, Baikoko kuwasindikiza Dar Modern

Hassan Kumbi 'Hassani Vocha' (kulia) mmoja wa waimbaji watakaotambulishwa Dar Modern. Msanii huyu alianzia Mkubwa na Wanae na pichani akiwa a Dogo Aslay na Bibi Cheka.
WASANII na makundi ya ngoma asilia ya Kibao Kata na Baikoko wanatarajiwa kunogesha onyesho la utambulisho  wasanii na nyimbo mpya za kundi la muziki wa taarab la Dar Modern 'Wana wa Jiji' waliorejea upya baada ya kimya cha muda mrefu.
Dar Modern lililowahi kulisimamisha jiji kwa nyimbo zake za 'Pembe la Ng'ombe' na 'Kitu Mapenzi', litafanya onyesho hilo Siku ya  Wapendanao, Magomeni Dar es Salaam.
Akizungumza na MICHARAZO, Kaimu Rais wa kundi hilo, Hassan Bakar alisema maandalizi ya onyesho hilo la Ijumaa  yamekamilika na iliyobaki ni kwa mashabiki wa burudani kujitokeza kwa wingi ukumbini kushuhudia Dar Modern mpya.
"Kila kitu kimekaa vyema na inasubiriwa Ijumaa mashabiki kuona nyota wapya wa kundi letu akiwamo msanii Hassani Vocha aliyeibuliwa na kituo cha Mkubwa na Wanae na kutamba na wimbo wa 'Vocha' alioimba na Dogo Aslay," alisema.
Bakar alisema katika kunkuogesha onyesho hilo, Dar Modern itasindikizwa na wasanii wa makundi ya unenguaji ya asilia ya Baikoko la Tanga na Kibao Kata.
"Burudani nyingine za kunogesha uzinduzi huo zitaongezwa wakati tukielekea kwenye onyesho hilo," alisema Bakar.
Dar Modern lililoanzishwa mwaka 2006 na baadhi ya wasanii waliokuwa Babloom Modern Taarab na Zanzibar, lilizimika baada ya baadhi ya nyota wake kujiengua likiwa linatikisa anga la muziki wa miondoko hiyo kupitia albamu zake karibu saba.
Albamu hizo ni pamoja na 'Ni Vijimambo Tu', 'Sote Twasaka Riziki', 'Gharika ya Moyo', 'Kitu Mapenzi','Toto la Kiafrika', 'Nauvua Ushoga' na 'Ndugu wa Mume Mna Hila'.
======================

No comments:

Post a Comment