STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 10, 2014

Barcelona yarejea kileleni, Messi moto mkali

At the double: Messi (left) scored twice to help Barcelona to a 3-1 win against Sevilla
Messi akishangilia moja ya mabao yake na Pedro
NYOTA wa Argentina, Lionel Messi anayichezea Barcelona jana alidhihirisha bado ni moto wa kuotea mbali baada ya kuisaidia klabu yake kuibuka na ushindi wa mabao 4-1 ugenini dhidi ya Sevilla.
Messi aliifungia Barca magoli mawili moja la kila kipindi huku bao la mapema la Alex Sanchez na lingine la jioni la Cesc Fabregas yalitosha kuirejesha mabingwa hao watetezi kileleni mwa msimamo waking'oa Real Madrid na Atletico Madrid waliokuwa juu yao.
Barcelona wamerejea kileleni wakiwazidi wapinzani wao uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa, licha ya zote kulingana pointi 57.
Wenyeji ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Moreno katika dakika ya 15 kabla ya Sanchez kusawazisha dakika ya 34 na baadaye Messi kufunga bao la pili dakika ya 44.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na Messi kuongeza bao la tatu katioka dakika ya 55 kabla ya Fabregas kuhitimisha ushindi huo mnono kwa bao la dakika ya 87.

No comments:

Post a Comment