STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 9, 2014

Manchester Utd yazidi kuchechemea yabanwa nyumbani na Fulham

Darren Bent scores Fulham's equaliser
Darren Bent akiisawazishia Fulham bao dakika za lala salama
BAO la dakika ya 94 lililofungwa na Darren Bent liliiokoa Fulham dhidi ya kipigo toka kwa Mashetani Wekundu, Manchester United waliokuwa nyumbani kwao na kutoka sare ya 2-2.
Manchester United walioonekana kama wamevuna pointo zote tatu baada ya Robin van Persie na Michael Carrick kufunga mabao mawili na kuinyamazisha Fulham waliotangulia kupata bao la mapema la dakika 19 lililofngwa na Steve Sidwell.
Juan Mata alimtengenezea nafasi nzuri van Persie aliyefunga bao la kusawazisha dakika ya  78 kabla ya Carrick kuongeza la pili dakika mbili baadaye.
Hata hivyo mashabiki wa Old Trafford wakiamini wapata ushindi nyumbani, Bent alifunga bao la kusawazisha dakika nne za nyongeza za mchezo huo na kuipa pointi moja Fulham ugenini.
Matokeo hayo yameendelea kuiacha Manchester ambayo Jumatano itaifuata Arsenal iliyonyukwa jana na Liverpool kwa mabao 5-1, ikibaki nafasi ya saba ikiwa na pointi 41.

No comments:

Post a Comment