STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 9, 2014

Simba ya Logarusic yafa Tanga, Mbeya yainyuka Mtibwa, Coastal yatamba Tabora, Oljoro yanabwa na Kagera

Mgambo JKT
Mbeya City
Coastal Union iliyoshinda ugenini mjini Tabora dhidi ya Rhino Rangers
Mtibwa Sugar iliyokufa jijini Mbeya kwa mabao 2-1
BAO pekee la dakika ya 28 lililofungwa na Full Maganga limetosha kuiua 'Mnyama' Simba inayonolewa na kocha mwenye mbwembwe, Zdravko Logarusic mbele ya Mgambo JKT katika pambano la Ligi Kuu Tanzania Bara lililochezwa Mkwakwani Tanga.
Simba ambayo iliitafuna Mgambo iliyokuwa ikifundishwa na King Abdallah Kibadeni kwa mabao 6-0 licha ya juhudi za kutaka kurejesha bao hilo ilishindwa kabisa kuwapa raha mashabiki wake kwa kukubali kipigo cha pili kwa msimu huu na cha kwanza chini ya Logarusic tena kwa timu kibonde ya Mgambo.
Huo ni ushindi wa pili mfululizo kwa Mgambo JKT ambayo ilikuwa ikiburuza mkia kwa kipindi kirefu baada ya wiki iliyopita kuicharaza Ashanti United uwanja wa cha Chamazi.
Ushindi huo umeifanya timu hiyo inayonolewa na kocha mpya Bakar Shime imefikisha pointi 12 huku Simba ikisaliwa na 31 na kushuka nafasi ya nne iliyokuwa awali baada ya Mbeya City kushinda mabao 2-1 dhidi ya Mtibwa Sugar mjini Mbeya.
Bao la Mtibwa lilifungwa na Jamal Mnyate kabla ya Mbeya kurudisha bao kupitia na Peter Mapunda kwa kichwa na bao la ushindi  lilifungwa na Amani Kibokile. Dakika mbili kabla ya kumalizika mchezo Mtibwa ilipata bao la kusawazisha ambalo hata hivyo lilikataliwa na mwamuzi Israel Mkongo.
Mechi nyingine zimeshuhudia Coastal Union ikipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji wao Rhino Rangers ya Tabora kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, huku Oljoro JKT ilibanwa nyumbani na Kagera Sugar na kutoka nao sare ya 1-1.

No comments:

Post a Comment