STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 9, 2014

Adebayor aipaisha Spurs, waishusha Everton

Emmanuel Adebayor
Adebayor akipongezwa na Paulinho baada ya kufunga bao pekee dhidi ya Everton

Tottenham 1-0 EvertonMSHAMBULIAJI kutoka Togo Emmanuel Adebayor jioni hii ameiwezesha Tottenham Hotspur baada ya kufunga bao pekee lililoiwezesha kuizima Everton na kurejea kwenye nafasi ya tano katika msimamo wa Ligi Kuu ya England.
Adebayor alifunga bao hilo lililokuwa la tano kwake msimu huu kwenye ligi hiyo katika dakika ya 65 akimalizia kazi nzuri ya Kyle Walker na kumtungua Tim Howard na kuifanya Spurs kufikisha pointi 47 na kuwa nyuma ya Liverpool yenye pointi 50.
Everton waliokuwa wakishika nafasi ya tano kabla ya mchezo huo, imeshuka hadi nafasi ya sita ikisaliwa na pointi zake 44.
Muda mchache ujao, Manchester United wanaokamata nafasi ya saba watakuwa uwanja wake wa nyumbani wa Old Trafford kupepetana na Fulham katika pambano jingine la ligi hiyo.

No comments:

Post a Comment