STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 9, 2014

KMKM yawa Urojo Ethiopia kama Chuoni Zimbabwe

KMKM ya Zanzibar
KLABU za Zanzibar zimeendelea kuwa urojo baada ya jioni hii KMKM kutandikwa mabao 3-0 na Dedebit ya Ethiopia katika Ligi ya Mabingwa Afrika kama ilivyokuwa 'ndugu' Chuoni nchini Zimbabwe jana kwenye Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya wenyeji wao How Mine.
Kwa mujibu wa matokeo kutoka Addis Ababa, wenyeji walipata mabao yao katika vipindi vyote viwili, hadi mapumziko waliongoza kwa bao 1-0 lililoifungwa na Dawit Fekadu dakika ya 16.
Kipindi cha pili kilikuwa kigumu kwa KMKM baada ya kuongezwa mabao mengine mawili yaliyofungwa na Shimekit Gugsa dakika ya 52 kabla ya Micahel George kumalizia kazi dakika sita kabla ya pambano hilo kuisha.
Kwa matokeo hayo klabu za Zenji zimeendelea kuwa wasindikizaji katika michuano ya kimataifa kwani KMKM italazimika kupata ushindi wa mabao 4-0 ili kusonga mbele, kazi ambayo pia inayo Chuoni iliyopigwa 4-0 na How Mine ya Zimbabwe jana na kuonekana ni ndoto kushinda nyumbani 5-0.

No comments:

Post a Comment