STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 9, 2014

Simba, Mbeya City kuombeana mabaya leo VPL?

Mbeya City
Simba
LICHA ya kwamba zitakuwa kwenye viwanja tofauti, lakini timu za Simba na Mbeya City zitakuwa zikiombeana mabaya watakapokuwa wakiumana kuwania pointi tatu ili kujiweka pazuri kwenye msimamo.
Simba watakuwa ugenini kuuamana na Mgambo JKT, wakati Mbeya itakuwa nyumbani uwanja wa Sokoine kuumana na Mtibwa Sugar.
Mechi hizo mbili kati ya nne zinazochezwa leo zinafuatiliwa kwa karibu kutokana na timu hizo kulingana pointi na zikifukuzana kwenye msimamo unaoongozwa na Azam ambayo leo itakuwa na majukumu ya kimataifa katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Ferroviario de Beira ya Msumbiji.
Timu hizo zina pointi 31 kila mmoja na zinatofautiana uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa na kila mmoja watakuwa wakiwaombea wenzao wateleze ili kukalia nafasi ya tatu na kuwasogelea Yanga waliopo nafasi ya pili na pointi zao 35.
Kocha msaidizi wa Simba Seleman Matola amesema timu yake imepania kupata ushindi katika mchezo wa leo wa ligi kuu ya soka ya Bara dhidi ya Mgambo JKT kwenye Uwanja wa Mkwakwani, hasa baada ya kupata sare kwenye mechi iliyopita dhidi ya Mtibwa Sugar.
"Ile sare ilimuuma kila mtu kuanzia wachezaji mpaka benchi la ufundi," alisema Matola.
Aidha, alisema kuwa hakuna majeruhi kwenye kikosi chake na kila mchezaji amepewa majukumu kuhakikisha wanapata pointi tatu. Mgambo inashika mkia katika msimamo wa ligi kuu ikiwa imeshinda mara mbili katika michezo 16 mpaka sasa.
Matola alisema kupoteza mchezo au kutoka sare wakati wapinzani wao wakipata ushindi kutawaweka katika mazingira magumu.
"Mbio za ubingwa ni ngumu hivyo hatutakiwi kupoteza mchezo sasa hivi... tunajua Mgambo wanacheza mpira wa nguvu lakini tumejiandaa kuwakabili."
Mbeya wenyewe watrakuwa na kibarua kigumu kwa Mtibwa Sugar na kocha wake, JUma Mwambusi amenukuliwa akisema wamejiandaa kushinda nyumbani baada ya kuteleza ugenini mvele ta Yanga.
Mbeya City, 'ilitenguliwa udhu' na Yanga kwa kufungwa kwa mara ya kwanza kwenye ligi hiyo iliyoipanda msimu huu baada ya kunyukwa bao 1-0 kwenye uwanja wa Taifa wiki iliyopita na kutibua rekodi yao waliyokuwa wanachuana na Azam ambayo ndiyo pekee sasa haijapoteza mchezo wowote katika ligi hiyo.
Mbali na mechi hizo mbili zinzofuatiliwa, leo pia kutakuwa ni michezo mingine miwili Oljoro JKT kuikaribisha Kagera Sugar uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha na Rhino Rangers kuikaribisha Coastal Union mjini Tabora katika pambano litakalochezwa uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.

No comments:

Post a Comment