STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 20, 2015

UTAMU WA KOMBE LA KAGAME WAZIDI KUNOGA DAR

https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AKh2imIAABZpVaY5ZwsQCBMD2%2BU&midoffset=2_0_0_1_4350124&partid=2&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000http://rushyashya.net/IMG/jpg/apr_fc_team_-_rwanda_-_kigalitoday-2-2.jpg
APR Rwanda
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/07/Yanga-leo-14.jpg
Yanga na Gor Mahia
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgU-pwUoReK1Inoqwa-tv9F7B4FsQQHzQW9GaG7wzubvb9SCAbF6zgGuLW0T-HTTo2ede7ls9zqJuGTrYNNSoghMV8GO4-5kfnAbuNX1yjWmHghK_qRzBu2MQ1YkUVYSo-N7z6p23PgLzs/s640/426464_358635040821389_1508036080_n.jpg
Al Shend
http://kabumbu.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/kikosi-azam-fc.jpg
Azam ya Tanznaia Bara
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiYr-ePKerYIvN49hCZ9IJI-ICEdPieA86ey85RJHvQ131iGA6GEbCXWWbDogjLkjX3y6u7CQrhi07Wnmkj3cDy2Drr-O8hj23no_e0NxN6qDxt_0KSgzSb0084QpabXSEI7dIMJoRXD4bc/s1600/1385637_526389100785782_1638137288_n.jpg
Telecom ya Djibout
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg3v7qvqTyHyaPiHb4iJPQ2UjF7MIw0nVpNbqWGraZLfn3zrJ6t9J4bGJ0Ok268cn_goKj9RqzWVvhzIbNvWOTsBfGmrrJGfaTXfZfAcFez2kVA97hfblC6PDlqUiHoUIKjm5SeoML2U9q_/s1600/IMG_9898.JPG
KMKM ya Zanzibar
http://entebbenews.com/wp-content/uploads/2014/09/KCCA-Mulindwa-9.jpg
KCCA ya Uganda
Kikosi cha Yanga

Kikosi cha Gor-Mahia

Mchezaji wa Yanga, Amis Tambwe akiwa chini huku wachezaji Collins Okoth (kulia) na Harun Shakava (kushoto) wa Gor Mahia ya Kenya wakiwania mpira wakati wa mchezo wa ufunguzi wa mashindano ya Kombe la Kagame uliochezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo. Yanga imefungwa mabao 2-1.
Mashabiki wa Yanga

MICHUANO ya Kombe la Kagame imezidi kushika kasi ikiwa inaingia siku yake ya tatu leo tangu yalipofunguliwa rasmi siku ya Jumamosi, huku Al Khartoum ya Sudan ikitoa onyo kwa kuopata ushindi wa kishindi mchana huu dhidi ya Telecom ya Djibout.
Wawakilishi hao wa Sudan waliokuwa sambamba na Al Shandy kuchukua nafasi za mabingwa watetezi Al Merreikh na Al Hilal waliitandika bila huruma Telecom kwa mabao 5-0 na kukwea kileleni mwa Kundi A, ingawa kwa sasa Gor Mahia inayokamata nafasi ya pili na KMKM waliopo nafasi ya tatu wakiendelea kutifuana kwenye Uwanja wa Taifa.
KMKM ambayo ilichukuliwa poa katika kundi hilo, inaendelea kuonyesha kuwa haisindikizi mtu kwani ilitanguliwa kufungwa bao la kwanza na Gor Mahia iliyowazamisha Yanga kwa mabao 2-1 katika pambano la ufunguzi juzi, lakini ikakomaa na kulirejesha dakika tisa baadaye.
Wakenya walipata bao la mapema dakika ya tatu kupitia Meddie Kagere aliyemaliza pande tamu la Michael Olunga ambao ulimbabatiza beki mmoja wa KMKM na kumpoteza kipa wao, lakini Simon Mateo alifunga bao dakika ya 12 tu ya mchezo na muda huu wametoka kukosa bao la wazi.
Mpaka sasa wakati karibu timu zote zikiwa zimeshacheza mechi moja moja, Yanga na Telecom ndio wanaoburuza mkia katika kundi A zikiwa hazina pointi, ingawa Yanga wanakamata nafasi ya nne.
Katika Kundi B, APR ya Rwanda inaongoza msimamo baada ya kuishinda Al Shandy kwa bao 1-0 katioka mchezo wa kwanza, huku timu za Heggan ya Somalia na LLB AFC ya Burundi zinafuatia baada ya jana kutoka suluhu ya kutofungana.
Malakia ya Sudan Kusini inaongoza kundi C ikiwa na pointi tatu sawa na Azam iliyoitambia KCCA ya Uganda jana, lakini wanatofautiana kwa mabao ya kufunga na kufungwa. Malakia iliitambia Adama City ya Ethiopia kwa bao 2-1, wakati Azam yenyewe iliishinda KCCA bao 1-0.
Mpaka muda huu unaosoma blogu hii jumla ya mabao 18 yameshatinga wavuni kwa mechi 8 zilizokwisha kucheza mpaka sasa baada ya jioni hii Gor Mahia kuitambia KMKM kwa mabao 3-1.


Utamu wa michuano hiyo upo hivi kwa mwaka huu wa 2015
MAKUNDI:

KundiA: Yanga-Tanzania, Gor Mahia-Kenya, Khartoum-Sudan, Telecom-Djibout, KMKM-Zanzibar
Kundi B: APR-Rwanda, Al Shandy-Sudan, LLB-Burundi, Heegan-Somalia,
Kundi C: Azam-Tanzania, Malakia-Sudan Kusini,  KCCA- Uganda, Adama City- Ethiopia.

Viwanja:
Taifa- Temeke
Karume-Ilala


MATOKEO:

APR              1-0  Al Shandy
KMKM           1-0  Telecom
Yanga           1-2  Gor Mahia
Adama City   1-2  Al Malakia
LLB              0-0   Heegan
Azam           1-0   KCCA
Telecom        0-5  Al Khartoum
Gor Mahia     3-1  KMKM
 

MSIMAMO:
Kundi A:
                      P  W  D  L   F  A PtsGor Mahia       2   2   0  0   5  2  6Al Khartoum    1   1   0  0   5  0  3
KMKM             2   1   0  1   2  3  3
Yanga             1   0   0  1   1  2  0
Telecom          2   0   0  2   0  6  0

Kundi B:
                     P  W D  L  F  A Pts
APR               1   1  0  0  1  0  3
LLB AFC         1   0  1  0  0  0  1
Heegan          1   0  1  0  0  0  1
Al Shandy      1   0  0  1   0  1  0

Kundi C:

                     P  W D  L  F  A  Pts
Al Malakia       1  1 0  0  2  1   3
Azam              1  1 0  0  1  0   3
Adama City     1  0  0  1  1  2  0
KCCA              1  0  0  1  0  1  0

Wafungaji:

3-Michael Olunga         (Gor Mahia)

2- Salah Bilal               (Al Kahrtoum)
1- Ousmaila Baba         (Al Khartoum)
    Haruna Shakava       (Gor Mahia)
    Michael Olunga         (Gor Mahia)
    Kirkir Glay (og)         (Gor Mahia)
    John Bocco               (Azam)
    Bizimana Djihad        (APR)
    Takele Elemayehu     (Malakia)
    Samuel Ssekamatte  (Malakia)
    Jafar Delil                 (Adama City)
    Juma Mbwana           (KMKM)
    Wagdi Abdallah         (Al Khartoum)
    Murwan Abdallah      (Al Khartoum)
    Meddie Kagere          (Gor Mahia)
    Simon Mateo            (KMKM)
    Meddie Kagere          (Gor Mahia)
RATIBA
KESHO Jumanne

Saa 8 Mchana  Al Shandy vs LLB-Karume
Saa 10 Jioni     Heggan vs APR-Karume
Saa 10 Jioni     Malakia vs Azam-Taifa

Jumatano

Saa 10 Jioni     Khartoum vs KMKM-Karume
Saa 8 Mchana  KCCA vs Adama City-Taifa
Saa 10 Jioni     Telecom vs Yanga-Taifa

Julai 23

Saa 8 Mchana  Hegaan vs Al Shandy-Taifa
Saa 10 Jioni     APR vs LLB-Taifa

Julai 24

Saa 8 Mchana  Khartoum vs Gor Mahia-Taifa
Saa 10 Jioni     KMKM vs Yanga-Taifa

Julai 25

Saa 8 Mchana  KCCA vs Malakia-Taifa
Saa 10 Jioni     Adama City vs Azam-Taifa

Julai 26

Saa 8 Mchana  Gor mahia vs Telecom-Taifa
Saa 10 Jioni     Yanga vs Khartoum-Taifa

Julai 27 Mapumziko
Julai 28-Robo fainali
B1 vs A3
A1 vs Best Looser

Julai 29
B2 vs C2
Ca vs A2

Julai 30-Mapumziko

Julai 31-Nusu Fainali
Winner B2/C2 vs C1/A2
    ""      B1/A3 vs A1/Best Looser
Agosti 01-Mapumziko

Agosti 02-Fainali

No comments:

Post a Comment