STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 20, 2015

Stewart afungka mbinu walizoizamisha KCCA

Stewart Hall akiteta na Migi
KOCHA Stewart Hall ni mjanja sana, baada ya kufichua siri ya kuwaanzisha viungo wengi na kucheza soka la kujihami na kushambulia kwa kutumia mipira mirefu. Akizungumzia mbinu zake, Hall alisema alilazimika kutumia mbinu hiyo kwa sababu wachezaji wake wengi bado hawapo fiti. “Tupo katika kipindi cha maandalizi ya mwanzo wa msimu, wachezaji wangu Kipre Tchetche, Didier Kavumbagu na Ramadhani Singano bado hawajawa fiti kwa asilimia mia, lakini naamini tutafika fainali.” alisema Hall Hall aliongeza kuwa timu inayomtisha zaidi ni Gor Mahia kwa sababu wamekuja wakati ligi ya Kenya inaendelea hivyo wachezaji wao wapo fiti.

No comments:

Post a Comment