STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 30, 2013

Coastal Unioni kutibua sherehe za ubingwa Jangwani kesho?




Coastal Union
KIVUMBI cha Ligi Kuu Tanzania Bara kinatarajiwa kuendelea tena kesho kwa michezo sita, likiwamo la Mabingwa wapya wa ligi hiyol, Yanga dhidi ya wagosi wa Kaya, Coastal Union walioapa kuwatibulia wana Jangwani sherehe zao za ubingwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Yanga ilitawazwa kuwa mabingwa Ijumaa iliyopita baada ya wapinzani wao wa karibu Azam kulazimishwa sare ya bao 1-1 na wagosi hao wa kaya waliokuwa kwenye uwanja wao wa Mkwakwani-Tanga.
Uongozi wa Yanga na benchi la ufundi la timu hiyo, liemsisitiza kuwa kunyakua kwao ubingwa hakuwafanyi walegeze makali yao ambapo tangu kuanza kwa duru la pili hawajapoteza mechi yoyote.
Hata hivyo kocha wa Coastal, Hemed Morocco amenukuliwa juzi akisema kuwa wamekuja Dar kwa ajili ya kutibua furaha ya ubingwa ya Yanga na kwamba mabingwa hao wasitarajie mteremko kwani lengo lao kuona wakimaliza ligi wakiwa kwenye Tatu au Nne Bora.
Wakati Yanga na Coastal zikitambiana hivyo kabla ya kuvaana kesho Dar, michezo mingine itakayochezwa kesho ni pamoja na lile la Mtibwa Sugar dhidi ya 'vibonde' Agfrican Lyon ambayo imeshashuka daraja, japo bado hawajatangazwa rasmi na TFF kama desturi.
Timu hizo zitaumana kwenye uwanja wa Manungu Complex, Turiani, ambapo Mtibwa itakuwa ikisaka pointi za kuwafukuzia ndugu zao, Kagera Sugar waliopo nafasi ya tatu katika msimamo.
Kagera wenyewe watakuwa ugenini mjini Morogoro kuvaana na Polisi Moro ambayo kama ilivyo kwa Lyona na Toto ni kama zimeshajikatia tiketi ya kurudi Ligi Daraja la Kwanza ilikoicheza msimu uliopita kabla ya kupanda Ligi Kuu msimu huu.
Polisi na Lyon zote zina pointi 19 kila moja na hata zikishinda mechi zao za mwisho zitafikisha pointi 25 ambazo zimerukwa na asilimia kubwa ya timu zinazoshiriki ligi hiyo itakayofikia tamati yake Mei 18.
Pambano jingine la kesho litazikutanisha timu za maafande za Ruvu Shooting itakayokuwa nyumbani kuwakabili wageni wao JKT Oljoro kwenye uwanja wa Mabatini-Mlandizi Pwani.
Tayari Afisa Habari wa Ruvu, Masau Bwire alemchimba mkwara kwamba vijana wao wapo tayari kutoa dozi kwa Oljoro kabla ya kuwakabilia Simba Jumapili kwenye uwanja wa Taifa, baada ya mechi yao ya awali kusogezwa mbele kitatanishi dakika za lala salama kabla ya kuanza kwake.
Bwire alisema lengo lao ni kuhakikisha mechi zao nne zilizosalia wanazishinda zote na kuwa fanya wamalize msimu wakiwa na pointi 42 zinazoweza kuwaweka katyika nafasi ya Tatu Bora au Nne msimu huu.
Mchezo wa mwisho kwa kesho utachezwa kwenye uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam kwa maafande wa JKT Ruvu watakapowakaribisha askari wenzao wa Magereza, Prisons-Mbeya ambazo hazina cha kupoteza kwenye msimamo wa ligi hiyo kutokana na kwamba zote hazina nafasi ya ubingwa wala kushuka daraja.
Msimamo wa Ligi hiyo kwa sasa ni kama ifuatayvyo:


                             P      W     D     L     F      A     D     Pts
Young Africans      24    17     5     2     44     13    31    56
Azam                    24    14     6     4     42     20    22    48    
Kagera Sugar        23    11     7     5     26     18     8     40     
Simba                   23    10     9     4     34     22    12     39
Mtibwa Sugar       24     9      9     6     27     24     3      36   
Coastal Union       24     8    10     6     24     21     3      34    
Ruvu Shooting      23     8     6      9     21     22     -1     30     
JKT Oljoro FC    24     7     7     10    22     28     -6     28     
Tanzania Prisons   24     6     8     10    14     21     -7     26    
Ruvu Stars           24      7     5     12    20     37     -17   26
JKT Mgambo       23     7     4     12    15     23     -8     25
Toto Africans       25      4     10   11    22     33     -11    22
African Lyon        24      5     4     15     16    36     -20     19
Polisi Morogoro   24      3    10    11     12    23     -11     19    
             

No comments:

Post a Comment