STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 30, 2013

Mourinho na vijana wake kuvuna nini leo Ulaya?

http://www.footballtarget.com/wp-content/uploads/2012/11/real-madrid-vs-borussia-dortmund-match-preview-champions-league.jpg
KOCHA Jose Mourinho na vijana wake wa Real Madrid leo wana kibarua kizito cha kuudhibitishia dunia kwamba soka lina maajabu yake watakapowakaribisha Borussia Dortmund nyumbani kwao, Santiago Bernabeu katika nusu fainali ya marudiano wakiwa na deni la kipigo cha mabao 4-1 walichopewa ugenini.
Mourinho na vijana wake walichezea kichapo cha mabao 4-1 ugenini nchini Ujerumani katika pambano la kwanza la Nusu Fainali ya michuano hiyo na hivyo leo watalazimika kulipa kisasi ili  kutinga fainali na kusaka taji la 10 na la kwanza tangu mwaka 2002.

Madrid watahitajika kushinda mabao 3-0 ili kutinga fainali za Ulaya baada ya misimu kadhaa ya ukame wa taji hilo tangu ilipotwa mara ya mwisho mwaka 2002.
Hata hivyo huenda isiwe kazi rahisi kwa vijana wa Santiago Bernabeu kutokana na ukweli wapinzani wao wapo vyema msimu huu licha ya kutemeshwa taji la ubingwa wa Bundesliga na Bayern Munich.
Dortmund wanasaka heshima baada ya kutwaa taji hilo mara ya mwisho mwaka 1997, hivyo huenda hawatakubali kuipoteza nafasi waliyopata safari hii kwa mabao manne ya Robert Lewandowski aliyefunga katika pambano la awali wiki iliyopita.
Wakati hatma ya Madrid na Dortmund ikitarajiwa kufahamika usiku wa leo, mabingwa wengine wa zamani wa Ulaya, Barcelona na Bayern Munich zenyewe zitakuwa na kibarua kingine kesho nchini Hispania.
Barcelona iliyocheze kichapo cha aibu wiki iliyopita ugenini kwa kulala kwa mabao 4-0 itakuwa nyumbani kujaribu kutupa karata yake kwa wageni wao ambao msimu huu wanatisha kisoka barani Ulaya.
Ikiwategemea nyota wake kama Xavi, Iniesta, Cesc Fabregas na Lionel Messi, Barca itakuwa na kazi pevu kulipiza kisasi na kutaka kupenya katika pambano hilo ili kucheza fainali Mei 25 itakayochezwa kwenye uwanja wa Wembley, Uingereza.
Je, ni Wahispania au Wajerumani watakaoenda London kwenye fainali hizo? Tusubiri tuone maana soka lina maajabu yake.

No comments:

Post a Comment