STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 15, 2015

Hapana! Hii ni Barcelona kweli? Yapigwa 4-0 na Bilbao

Athletic Bilbao's defender Mikel San Jose points to the heavens after scoring an incredible goal to put the underdogs ahead
Wachezaji wa Bilbao wakishangilia mabao yao dhidi ya Barcelona
Gorka Iraizoz comes out to deny Luis Suarez as the former Liverpool man tries to round the home keeper and bring his side level
Suarez akijitahidi kuipiugania Barcelona, lakini wapi walilala 4-0
Mikel Balenziaga ushers the ball away from Messi as the home defence looked to minimise the impact of Barcelona's best player
Messi hakufurukuta kabisa
SIKU chache baada ya kufanikiwa kushinda UEFA Super Cup kwa mbinde kwa kushinda mabao 5-4 dhidi ya Sevilla, mabingwa wa Hispania, Barcelona imetoa ishara mbaya ya kwamba msimu huu huenda ikawa urojo baada ya usiku wa jana kupigwa 4-0.
Barca wamekumbana na kipigo hicho kwenye pambano la Super Cup la Hispania kuashiria kuanza kwa msimu mpya wa La Liga na klabu ya Athletico Bilbao waliokuwa uwanja wa nyumbani.
Mabao matatu ya Aritz Aduriz na jingine la Mikel San Jose kwenye Uwnaja wa wa San Mames Barria, yalitosha kuizima Barcelona licha ya kuwa na nyota wake kadhaa akiwamo Messi na Luis Suarez.
San Jose alianza kumtungua kipa Marc-Andre ter Stegen dakika ya 13 kabla ya Aduriz kufunga mabao mawili ya haraka haraka dakika za 53 na 62.
Aduriz akakamilisha hat-trick yake kwa bao la mkwaju wa penalti, baada ya beki Dani Alves kumchezea rafu. 

No comments:

Post a Comment